BENKI ya Barclays nchini imezindua rasmi kwa mara ya kwanza nchini mfumo mpya wa utoaji huduma za kibenki bila kutumia karatasi au kujaza fomu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana asubuhi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Bw, Kumaran Pather alisema kuwa wanajivunia kuwa benki ya kwanza nchini kutumia mfumo wa utoaji wa huduma za kibenki kwa mfumo huo mpya.
 

Meneja Miradi waBenki ya Barclays Tanzania, Jane Mbwilo (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo mpya wa utoaji huduma za kibenki bila kutumia karatasi au kujaza fomu jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wengine kutoka  kushoto kwake ni, Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Bwana Kumaran Pather, Mkuu wa Operesheni za Kibenki, Sabiha Gulam na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Neem-Rose Singo.  
Alisema kwamba mfumo huo wa kutoa huduma za benki bila kujaza fomu au karatasi ni moja tu ya huduma mbalimbali ambazo benki hiyo inaleta katika kuboresha huduma zake kwa wateja.

“mfumo huu wa utoaji huduma za kibenki bila kutumia karatasi unachukua nafasi ya matumizi ya karatasi katika kupata huduma ikiwemo fomu mbalimbali za kutolea na kuchukulia pesa,” 

“uvumbuzi huu ni wa kisasa na tunajivunia kwa sababu wateja wetu sasa hivi wanatumia chini ya dakika tatu kuweza kukamilisha miamala yao ikiwemo kulipwa fedha taslimu, kuweka cheki, kutoa pesa na kubadili hundi kuwa pesa taslimu,” alisema Bw, Pather 

Bw, Pather aliongeza kuwa uvumbuzi huu umesaidia kupunguza gharama kwa kiasi kikubwa katika kuhudumia wateja na pia inapunguza muda wa utoaji wa huduma kwa wateja.

Alisema kwamba mfumo wa utoaji huduma bila kutumia karatasi inaweka hatua nzuri ya kuwezesha mteja achanganuae cheki wa mashine ya elektroniki na baadaye utasaidia cheki kukaguliwa na kifaa maalum, kupitiwa na kuidhinishwa na Benki kuu (Cheque truncation).

Kwa upande wake, Meneja Miradi wa Barclays Jane Mbwilo alisema benki hiyo inakuwa ya kwanza kutumia mfumo huu nchini Tanzania na kuwa benki ya kwanza kutumia mfumo wa kupitisha cheki kwa mitambo inayojiendesha yenyewe.

“Tumepiga hatua kubwa sana katika kuboresha huduma kwa wateja wetu na mfumo huu mpya wa kutoa huduma bila makaratasi, wateja wetu wote wanaweza kutumia mfumo huu katika matawi yote ya Barcalys nchini,” alisema
Aliongeza kuwa mkakati wa benki hiyo ni kutumia teknolojia ambayo itasaidia kurahisisha huduma kwa wateja pia na kupunguza gharama za uendeshaji wa benki.


Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.