WIKI Iliyopita Muungano wa asasi zisizo za kiserikali mbalimbali za kutetea haki za binadamu nchini kifupi AZAKI waliandaa mdahalo wa kwanza wa katiba jijini Dar es Salaam uliohudhuriwa na watu mashuhuri, vijana, wanafunzi wa kutoka vyuo vikuu mablimbali na kurushwa moja kwa moja na vituo kadhaa vya luninga hapa nchini, hongereni kwa kuwapa maarifa na uelewa watanzania wengi kuhusu mchakato unaoendelea wa kuandika katiba.
 
Mwenyekiti wa Kongamano la Katiba, Dk Ayub Rioba akizungumza na wajumbe mbalimbali waliohudhuria mdahalo ulioandaliwa na Muungano wa Asasi za Kiraia (Azaki) uliofanyika Dar es Salaaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa utetezi wa Haki za Binadamu, Onesmo Olengurumwa na Awadhi Ally Saidi aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya kukusanya maoni. Picha na Venance Nestory      

Kwa kutumia nafasi hiyo AZAKI ilitumia fursa hiyo kuwafunda watanzania kwamba kila tunapofikiria au kuzungumzia kuhusu katiba mpya, yanayojitokeza wazi kabisa ni Muundo wa Serikali, yaani mbili au tatu.


Kwa mujibu wa AZAKI pia kwamba wenye maslahi makubwa sana na katiba mpya ni CCM na UKAWA huku wananchi ambao kimsingi ndio katiba yao wakiwa wameachwa solemba na wimbi la wanasiasa wenye malengo yanayofanana hasa ni kutwaa madaraka na kupigiwa vingo’ra tu na kuu wa kuhabutubiwa kwisheeeeeeee.


Kwa mujibu wa AZAKI wanasema kwamba wananchi bado hawajawezeshwa kuifahamu Rasimu ya Pili ya Katiba, na kwamba mchakato wa Katiba mpya umepoteza mwelekeo na hauna tena maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.


Akizungumza katika mkutano wa AZAKI, aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Profesa Mwesiga Baregu alimtaka Rais Jakaya Kikwete kunusuru mchakato wa kupata katiba kwa kuwa yeye binafsi ndiye aliyeuvuruga.


“Mchakato mzima ulikwenda vizuri, lakini baada ya Kikwete kulihutubia Bunge Maalumu la Katiba, mwelekeo wa Bunge hilo ulibadilika na kuwa na msimamo wa chama,” amesema Profesa Baregu.


Amesema kuwa Rais Kikwete alikwenda kulihutubia Bunge kama kiongozi wa CCM, badala ya kiongozi wa nchi, ambapo aliweka msimamo wa chama chake wa kutaka Muundo wa Serikali mbili na kuwavuruga wajumbe ambao kimsingi ni wanachama wa CCM.


“Rais apate ujasiri akiwa kama kiongozi wa nchi na siyo kama kiongozi wa CCM, awahutubie wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na kuwataka wajadili Katiba ya wananchi na siyo ya chama wala yake binafsi,” aliongeza Baregu.



Baregu aliwataka wajumbe watumie miezi miwili iliyobaki kujipanga upya iwapo wana nia ya dhati ya kuendelea na mchakato huo, ili ipatikane Katiba bora ya wananchi akionya kwamba, tofauti na hapo Watanzania hawatakubali kuendelea kuburuzwa na misingi ya chama cha mapinduzi.


Kauli ya Baregu pia iliungwa mkono na Mwenyekiti wa Chama cha Sheria Zanzibar, Awadhi Ally Saidi ambaye ni pia ni miongoni mwa waliokuwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, aliyesema kuwa inafaa Rais awahutubie wajumbe na kuwakumbusha kuwa jukumu lao ni kujadili Rasimu ya Katiba ya kuipitisha na siyo kuondoa vipengele au kubadilisha rasimu au kufanya mambo kinyume na maoni ya wananchi.


“Ndiyo maana walipewa siku 70 kujadili Rasimu ya Katiba, lakini walitumia siku 21 kutunga kanuni ambazo zilitungwa na Baraza la Wawakilishi likishirikiana na Bunge la Muungano,” amesema.


Kwa upande wake, Mratibu wa Mtandao wa kutetea haki za binadamu, Onesmo Olengurumwa ambaye pia ni mwanasheria amesema kwamba makosa yalifanyika awali kwa kumuachia rais ateue wajumbe wa bunge la katiba.


“kwa kufanya makosa ya kumwachia rais ateue wajumbe wa bunge la katiba sasa bunge hilo limechepuka kutoka katika nafasi yake na kutaka kubadili maoni ya wananchi na kuweka maoni ya chama tawala,” amesema Olengurumwa

Amesema kwamba kwa sasa rais wan chi hana nafasi ya kurekebisha makosa maana ameshakosea wenye jukumu hilo kwa sasa ni wananchi wenyewe wa Tanzania kulirudisha bunge hilo kwenye mstari unaofaa.



Rais Jakaya Kikwete ameshauriwa kunusuru mchakato wa kupata Katiba Mpya ili usisimame kwa kuvua koti la Uenyekiti wa CCM na kubaki na Urais ili awaeleze wananchi nini cha kufanya kupata Katiba Mpya.


Ushauri huo umetolewa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na wasomi walioshiriki katika mdahalo wa Katiba uliofanyika jijini Dar es Salaam na Mwanza jana. Walisema kuwa Rais ana wajibu kuunusuru mchakato huo kwa kuwa yeye ndiye aliyeuvuruga kwa hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge Maalumu la Katiba iliyoonekana kuelemea upande wa chama chake CCM.



Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema Rais Jakaya Kikwete amekuwa kigeugeu juu ya Muundo wa Serikali za Muungano kama zilizopendekezwa kwenye Rasimu ya Kwanza na ya Pili ya Katiba.



Alisema kuwa Rais Kikwete alionyesha wazi kukubaliana na Muundo wa Serikali tatu, kwani kabla Rasimu ya Pili ya Katiba haijapelekwa kwenye Bunge Malaumu la Katiba ili kujadiliwa, alisaini kuonyesha kuwa amekubaliana na yaliyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.



Akihutubia kwenye Kongamano la Wazi na Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine



cha Mwanza (Saut) Dk Slaa alisema:



“Rais Jakaya Kikwete amekuwa kigeugeu, kwani yeye ndiye aliyesaini Rasimu ya Pli ya Katiba ili ikajadiliwe kwenye Bunge Maalumu la Katiba.” Aliongeza: “Kwa kuwa ndiye mtu wa mwisho kuruhusu rasimu hiyo ijadiliwe kwenye Bunge Malaamu la Katiba ni wazi alikubaliana na kilichopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyopendekeza Muundo wa Serikali Tatu, hivyo inashangaza kuona leo anageuka na kutaka Serikali mbili.”



Dk Slaa ambaye pia ni kiongozi katika Umoja wa Katiba ya Wananchi Nje ya Bunge (Ukawa), alisema kuwa katika mikoa 17 waliyozunguka na kufanya mikutano na wananchi, wamebaini kuwa Rasimu ya Katiba ya Pili wananchi hawaifahamu na kwamba hiyo ni njia ya CCM kuchakachua maoni yao yaliyomo kwenye rasimu hiyo, wakati wa kupiga kura za maoni.



Alisema wanatambua ujanja unaofanywa na CCM kutaka kupitisha mambo wanayoyataka wao, lakini wao watendelea kuwaelimisha wananchi ili watambue kwamba maoni yao ndiyo nguzo ya kuwapa Katiba bora na siyo vinginevyo.



“Tumefanya mikutoano mikoa 17, lakini kote tulipopita wananchi wametuambia hawaifahamu Rasimu ya Pili ya Katiba kutokana na janja ya CCM kuficha rasimu ya hiyo ili wananchi wasiifahamu. Kutokana na hilo  ni wazi kwamba wanataka kuchakachua maoni ya wananchi kwenye kura za maoni,”alisema Dk Slaa.



Akinukuu maneno kutoka katika hotuba ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliyoitoa mwaka 1995 Dk Slaa alisema: “Watu wapumbavu ni wale wanaoamini kwamba Katiba haibadiliki.”



Alisema lazima Katiba ibadilike na kwamba wananchi ndiyo wenye Katiba, hivyo siyo busara kutaka kuchakachua maoni yao na kuweka maoni ya chama au mtu binafsi.

Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.