![]() |
George Tawlon Manneh Oppong Ousman Weah Mwanajamii, Mwanasiasa, na mchezaji wa zamani aliyecheza kama mshambuliaji ,anatoka Liberia. |
Ilikuwa ni mwezi Desemba, mwaka 1995, ni pale FIFA ilipoitangazia dunia ya soka, kuwa George Weah amechaguliwa kwa kupigiwa kura kuwa mwanasoka bora wa dunia.

Na mwaka huo huo, George Weah akawa Mwanasoka Bora wa Ulaya, na haikuishia hapo, akatangazwa pia kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika! Mwaka mmoja mataji matatu!
George Weah alianza kusakata kabumbu nchini mwake Liberia kabla ya kuhamia klabu cha Monaco, na baadae Paris Saint Germain. Mwaka 1995 akaenda kwenye klabu ya Milan na ndipo akafikia kilele cha mafanikio yake katika soka. Kwenye uwanja wa nyumbani wa San Siro wa timu ya Milan, George Weah alikuwa mfalme aliyependwa sana na wapenzi wa Milan.

George Weah akagalagazwa na mwanamama Ellen Johnson - Sirleaf.
Post a Comment