Hayo yalisemwa na Kamishna wa Utawala na Utumishi wa Jeshi la Polisi nchini, Thobias Andengenye katika wakati akipokea kwa niaba ya mkuu wa jeshi hilo (IGP), msaaada wa tani 50 za saruji zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 12 kutoka Kampuni ya Saruji ya Twiga (TPCC), kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha polisi cha Mbweni    Malindi  nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Kamishna Andengenye alisema kuwa hata kama wananchi wakijenga nyumba imara lakini kuna umuhimu wa kuwepo kwa vituo vya polisi katika makazi ili kuweza kutoa msaada wa haraka pindi uhalifu utakapotokea.

"Kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, Ernest Mangu ambaye alipenda kuwepo mahali hapa nachukua nafasi hii kuipongeza kampuni ya Twiga Cement kwa msaada huu, makampuni na taasisi nyingine na bila kusahau juhudi za wananchi wa Kawe katika kuhakikisha kituo hiki kinakamilika haraka," alisema.

Akizungumza wakati akikabidhi saruji hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TPCC, Alfonso Rodriguez alisema msaada huo umewezeshwa kutoka na sera nzuri ndani ya kampuni ya kuisaidia jamii inayowazunguuka na pia wanayofanya nayo biashara.

"kama ilivyo kauli mbiu ya Twiga Cement isemayo 'Usalama Kwanza' ni matumaini yetu jamii ikiwa salama itakuwa rahisi kuleta maendeleo yao kiuchumi na pia kufanya kuwezesha biashara yetu iendelee vizuri," alisema.

Kwa upande wake Kamishna  wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam , Suleiman Kova aliwapongeza wakazi wa Mbweni kwa kutekeleza kwa vitendo dhana nzima ya ulinzi shirikishi.

Awali alizungumza katika hafla hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa kituo hicho, Reeves Ntalemwa  alisema uamuzi wa kujitolea kujenga kituo hicho kitakachogharimu sh milioni 700 hadi kukamilika ulioanzishwa na wananchi wenye umetokana na kuongezeka kwa matukio ya uhalifu katika eneo hilo linalopakana na Bahari ya Hindi.

Ukiacha kampuni ya Twiga, wadau wengine wa maendeleo waliotoa misaada mbalimbali kufanikisha ujenzi huo ni benki za CRDB PLC, NMB na NBC, wengine ni kampuni za VGK Ltd, Giant Hill, IPTL, HISAJE na Ulotu.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.