MAHAKAMA Kuu Kanda Ya Dar es Salaam, leo itaanza kusikiliza kesi  iliyofunguliwa na wanachama wa tatu wa  Timu ya Soka ya Simba,  ambao wanakomba mahakama hiyo  itoe amri ya Muda  ya Kuzuia  kufanyika  kwa uchaguzi Mkuu wa Timu  hiyo ambao umepangwa  kufanyika Juni 29 Mwaka huu.
Akizungumza na Tanzania Daima Jana mchana, Wakili wa wanachama  Hao,  Revocatus Kuuli alisema  uongozi wa Mahakama umempatia Jaji Augustine Mwarija kuisikiliza na inaanza kusikilizwa kusikilizwa Leo.

Endapo Jaji Mwarija atasikiliza Kesi hii Na.291/2014  Kama ilivyopangwa, itakuwa ni Mara yake ya pili kusikiliza Kesi ya aina hiyo. Mara ya Kwanza ilikuwa ni Mei 8 Mwaka  2010 ambapo Jaji  Mwarija akiwa na wa Mahakama hiyo alitoa amri ya  kubatirisha amri ya muda ya kuzuia uchaguzi mkuu wa klabu ya Simba uliofanyika Mei 9 mwaka 2010.

Amri ya kuzuia kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa simba iliyotenguliwa na jaji huyo ilitolewa Mei 6 mwaka 2010 na aliyekuwa Hakimu Mkazi Wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Amiceth Wambura ambapo Jaji Mwarija Alisema Amefikia uamuzi wa kutengua amri hiyo baada ya kubaini kuwepo Kwa dosari Katika amri ile ya Mahakama ya Kisutu.

Amri hiyo ilitolewa  saa 1:10 jioni na Jaji Agustine Mwarija baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili zilizokuwa zinavutana katika kesi iliyokuwa imefunguliwa na Michael Wambura dhidi ya mwenyekiti wa klabu ya Simba, wa wakati huo, Hassan Dalali, kuruhusu uchaguzi huo kuingiliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Juni 23 mwaka huu, wananchama Hao watatu kupitia Wakili wao Kuuli walifungua   mahakamani hapo Maombi hayo madogo, Na.291/2014  Josephat Waryoba, Said Lly Monero na Hassan Hassan, ambao wanamshitaki Rais wa Timu ya Simba, Ismail Aden Rage na Bodi ya Udhamini ya Timu  hiyo.

Kwa mujibu wa hati hiyo inayonyesha walalamikaji wana jumla ya Madai matatu ambayo dai la kwanza wakiomba Mahakama hiyo itoe amri ya kuwazuia wadaiwa kuitisha uchaguzi Mkuu uliofangwa kufanyika Juni 29 Mwaka huu.

Wakili Kuuli analitaja ombi la pili ni wanaomba jumla ya wanachama 66 waunganishwe Kwenye Kesi hiyo ili nao wawe walalamikaji dhidi ya wadaiwa   kwasababu wadaiwa ambao Rage na Bodi ya Wadhamini wamevunja   Katiba ya Simba , taratibu za uchaguzi na  na maadili ya uchaguzi , kadi za uanachama za wanachama hao zimearibiwa.

Wakili Kuuli alidai kuwa mdaiwa wa kwanza Kamati ya Utendaji ya Simba walishindwa kuweka sawa Kamati ya Maadili  ya simba  Kama inavyotakiwa  na Katiba ya Timu  hiyo na Kanuni za uchaguzi za TFF.

Alidai Kwa  vitendo hivyo wadaiwa hao  wamevunja taratibu  zote  za uchaguzi  na kwamba Hakuna Chombo Cha klabu ya Simba  ambacho kimepewa madaraka ya kusimama a masuala ya rufaa ya Maadili ya wanachama wake  na kwamba rufaa zote zote zinazohusu Maadili zinasimamiwa na mdaiwa wa pili(Bodi ya wadhamini ya simba),  nakwasababu hiyo wanaiomba Mahakama hiyo itafsiri Hilo.

" Japo Kuwa maelekezo toka TFF  kwenda mdaiwa wa kwanza (rage) ya
Yaliyomtaka Rage aweke  sehemu ya  Kamati ya Maadili , Rage  alishindwa kutekeleza maelekezo hayo KWA Madai Kuwa  robo  Tatu ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji wa Timu hiyo , wanatuhumiwa KWA makosa ya utovu wa Maadili .

" Barua ya TTF kwenda KWA Rage  ya Mei   29 Mwaka huu ,na barua ya Mwenyekiti wa Simbaya Juni 17 Mwaka huu ambayo alikuwa akimjibu Rais wa  TFF, Jamal Malinzi ni  ambazo tumeziambatanisha katika hati yetu ya madai kama vielelezo ili mahakama itoe tafsiri ya sheria " alidai wakili huyo.

Aidha walalamikaji hao wanadai Kuwa Kamati ya Uchaguzi ya Simba ipo kinyume na Katiba ya Timu ya Simba Kwani Kamati hiyo Ina baadhi ya wanachama ambao walioteuliwa Na Kamati ya Utendaji  na waliondolewa na Rais wa Timu hiyo  Katika Kamati hiyo kinyume Cha Sheria .

Pia wamedai Kuwa Kamati ya uchaguzi ya simba  haina mamlaka ya Kamati ya Maadili  ya kuwandoa  baadhi ya wagombea Katika mchakato wa uchaguzi Mkuu Kwani Kamati ya uchaguzi wa kuwachuja wagombea  pekee na suala la utovu wa Maadili  na nidhamu ya mgombea jukumu Hilo limekabidhiwa  Kwenye Kamati ya Maadili peke na siyo Kamati ya Uchaguzi .

"Kwa Sababu hiyo tunaimba Mahala hii itamke Kuwa utaratibu wote wa kuendesha uchaguzi ndani Timu  ya Simba  ni batiri  kwasababu umekiuka Katiba ya Simba" Alidai Wakili  Kuuli.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Juni 25 Mwaka 2014.

Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.