Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano kwa mwaka 2014 ambao waliomaliza kidato cha nne mwaka 2013
Wanafunzi waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti kwenye shule walizopangiwa kuanzia tarehe 10 Julai 2014 na mwisho wa kuripoti ni tarehe 30 Julai 2014. Aidha, hakutakuwa na mabadiliko ya wanafunzi kubadilishiwa shule walizopangiwa, hivyo wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangiwa kama inavyoonekana katika matokeo haya.
SOMA TAARIFA YA UCHAGUZI WA WANAFUNZI KUINGIA KIDATO CHA TANO HAPA
MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO MWAKA 2014


Wasichana Shule Zote

Wavulana Shule Herufi A-L

Wavulana Shule Herufi M-Z

Source by www.pmoralg.go.tz



2.0 WATAHINIWA WALIOFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE, MWAKA 2013

Jumla ya watahiniwa 427,679 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2013, wakiwemo wasichana 199,123 sawa na asilimia 46.56 na wavulana 228,556sawa na asilimia 53.44. Kati yao watahiniwa 404,083 sawa na asilimia 94.48 walifanya mtihani na watahiniwa 23,596 sawa na asilimia 5.52 hawakufanya mtihani huo.

2.1 Watahiniwa wa Shule (School Candidates)

Kwa Watahiniwa wa Shule, watahiniwa 367,163 walisajiliwa kufanya mithanikati yao wavulana
ni 198,099 na wasichana ni 169,064. ambapo watahiniwa 352,614sawa na asilimia 96.04 walifanya mtihani; kati yao wasichana walikuwa 162,412 sawa na asilimia 96.07 na wavulana 190,202 sawa na asilimia 96.01. Watahiniwa14,549 sawa na asilimia 3.96 hawakufanya mtihani kwa sababu mbalimbali.

2.2 Watahiniwa wa Kujitegemea (Private Candidates)

Kati ya watahiniwa60,516 wa kujitegemea waliosajiliwa kufanya mtihani, watahiniwa 51,469 sawa na asilimia 85.05 walifanya mtihani na watahiniwa 9,047 sawa naasilimia 14.95 hawakufanya mtihani kwa sababu mbalimbali.

Jumla ya watahiniwa 235,227 sawa na asilimia 58.21 ya watahiniwa waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2013 walifaulu. Mwaka 2012 watahiniwa waliofaulu walikuwa 185,940 kati ya 431,650 waliofanya mitihani; hii ni sawa na asilimia 43.08. Matokeo haya yanaonesha kuwa mwaka 2013 ufaulu umeongezeka kwa asilimia 15.13.

3.1 Ufaulu wa Watahiniwa wa Shule

Mwaka 2013 Watahiniwa wa Shule waliofaulu ni 201,152 sawa na asilimia 57.05 ya watahiniwa 352,614 waliofanya mtihani. Kwa mwaka 2013 kuna ongezeko la ufaulu wa watahiniwa 41,405, sawa na asilimia 25.91 ikilinganishwa na ufaulu wa mwaka 2012 ambapo watahiniwa 159,747 walifaulu.

3.2 Ufaulu wa Watahiniwa wa Kujitegemea

Takwimu zimeonesha kuwa kumekuwa na ongezeko la ufaulu kwa watahiniwa wa kujitegemea kutoka 26,193, sawa na asilimia 43.07 mwaka 2012 hadi kufikia watahiniwa 34,075, sawa na asilimia 66.21 kwa mwaka 2013; Kwa kulinganisha na mwaka 2012 lipo ongezeko la asilimia 30.09 kwa ufaulu wa watahiniwa wa kujitegemea.

Ufaulu wa watahiniwa wa shule kwa mwaka 2013 katika madaraja ya I -III umefikia watahiniwa 71,527 sawa na asilimia 20.28 ya watahiniwa waliofanya mtihani Tanzania Bara.Hivyo kuna ongezeko la ufaulu wa asilimia 106.73 ikilinganishwa na matokeo ya ufaulu kwa mwaka 2012, kwa kuwa watahiniwa wa shule waliofaulu katika madaraja I-III kwa mwaka huo walikuwa 34,599 sawa na asilimia 9.67 ya watahiniwa waliofanya mtihani.

5.0TARATIBU ZA UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO 2014.

Kulingana na utaratibu uliowekwa na Serikali, mwanafunzi anayeomba kuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari kidato cha tano na vyuo vya Ufundi, hulazimika kujaza ‘Selform’ ambayo ndiyo fomu rasmi ya maombi. Kwa kutumia fomu hiyo, mwanafunzi huchagua maombi matano ya tahasusi (Combinations)za masomo anayotaka kusoma na shule anayotarajia kujiunga nayo kwa kila chaguo.
Kamati ya uchaguzi humpanga mwanafunzi katika machaguo yake ya masomo na shule kwa kuanzia na chaguo la kwanza. Kama mwanafunzi atakuwa hana sifa katika machaguo yote aliyoomba, mwanafunzi husika hupangiwa chaguo la somo alilofaulu zaidi na katika shule iliyopo karibu na wilaya yake ya makazi kulingana na tahasusi na nafasi zilizopo katika shule husika.

6.0 IDADI YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUINGIA KIDATO CHA TANO

Jumla ya Wanafunzi 54,085 sawa na asilimia 75.61 ya wanafunzi 71,527 waliostahili kuingia Kidato cha Tano Tanzania Bara kwa mwaka 2014 wamechaguliwa; hilo ni ongezeko la wanafunzi 20,402 kwa kulinganisha na wanafunzi 33,683 waliochaguliwa mwaka 2013. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 2014 wavulana ni 31,352na wasichana ni 22,733.

Wanafunzi wamechaguliwa kujiunga kidato cha Tano katika jumla ya shule 241 zikiwemo shule 33 zilizopangiwa wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka 2014.

Nawashukuru sana wadau wote wa elimu katika Halmashauri mbalimbali kwa kuimarisha miundombinu ya shule hizo, ikiwemo maabara.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha Tano 2014 ni kutoka shule za serikali na zisizo za serikali. Kati yao wavulana 14,826 sawa na asilimia27.41wamechaguliwa kusoma masomo ya sayansi na wavulana 16,526 sawa na asilimia 30.56 wamechaguliwa kusoma masomo ya sayansi ya Jamii. Aidha,wasichana 7,859 sawa na asilimia 14.53wamechaguliwa kusoma masomo ya sayansi na wasichana 14,874 sawa na asilimia 27.50 wamepangwa kusoma masomo ya Sayansi ya Jamii.

Nawapongeza walimu wote kwa juhudi walizozifanya katika ufundishaji kwa kuzingatia mbinu za ufundishaji walizopata kupitia mpango wa mafunzo kazini (INSET)kwa walimu wa sayansi na lugha (Kiswahili na Kiingereza) unaosimamiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Ofisi ya WaziriMkuu, Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa. Aidha nawapongeza wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi. Hali hiyo inaonesha kuwa jitihada za Serikali za kuhamasisha vijana kusoma masomo ya Sayansi zimeanza kuzaa matunda.

Natoa wito kwa wanafunzi wa jinsi zote kujisomea kwa bidii masomo yote, yakiwemo ya Sayansi na Sayansi ya Jamii, kwani yanategemeana. Walimu wa masomo ya Sayansi, Sayansi ya Jamii na Hisabati wanakumbushwa kutumia mbinu shirikishi za kitaalam na kisaikolojia katika kufundisha ili kuwavutia wanafunzi wengi zaidi kusoma na kufaulu mitihani yao. Aidha walimu wa masomo ya Sayansi, waendelee kuwahamasisha wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi wakiwemo wanafunzi wa kike. Aidha, wanafunzi wa kike wanapaswa kujiamini kuwa wanaweza masomo yote yakiwemo ya Sayansi, kwani siri ya kujifunza ni utayari.

7.0 WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA VYUO VYA UFUNDI, MWAKA 2014

Jumla ya wanafunzi 472wakiwemo wavulana 355na wasichana 117
wamechaguliwa kujiunga na Vyuo vya Ufundi. Idadiya wanafunzi hao imepungua kutoka 530 mwaka 2013 hadi 472 mwaka 2014 kwa sababu kwa sasa vyuo hivyo vimeanza kuchukua wanachuo wa shahada ya kwanza. Aidha, kutokana na ufaulu kuongezeka idadi ya wanafunzi wa kike waliochaguliwa kujiunga na vyuo hivyo imeongezeka kutoka wanafunzi 114 mwaka 2013 hadi wanafunzi 117mwaka 2014 sawa na ongezeko la asilimia 2.63.

Natoa wito kwa wanafunzi kuendelea kusoma kwa bidii masomo ya sayansi ili mwakani idadi ya wanafunzi wanaojiunga na mafunzo ya ufundi iongezeke ili Taifa lipate wataalam wa kutosha wa ngazi zote.

8.0 SABABU ZA WANAFUNZI KUKOSA KUCHAGULIWA KUINGIA KIDATO CHA TANO
Jumla ya wanafunzi 16,800 wakiwemo watahiniwa wa kujitegemea 10 waliokuwa na sifa za msingi hawakuchaguliwa kwa sababu mbalimbali zikiwemo: ufinyu wa nafasi za shule za Kidato cha Tano (wanafunzi 16,400) na kukosa tahasusi - Combination (wanafunzi 400).

Serikali inatarajia kufanya uchaguzi wa awamu ya pili baada ya kubaini nafasi zitakazokuwa wazi zinazotokana na wanafunzi ambao hawakuripoti awamu ya kwanza. Aidha, Serikali imeweka utaratibu wa kuwapatia nafasi ya kusoma kidato cha Tano na cha Sita kwa pamoja na shahada ya Ualimu wanafunzi wenye sifa.

Shule za Kidato cha Tano na Sita zinatakiwa kuwa na mahitaji ya msingi, ikiwemo miundombinu yenye uwiano sahihi wa vyoo, bafu, vyumba vya madarasa, bweni, jiko, bwalo, maktaba, maabara, chumba cha Jiografia; pamoja na samani kulingana na idadi ya wanafunzi.

Shule zenye Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne ambazo zinahitaji kuanzisha kidato cha Tano, zinatakiwa kuwa na miundombinu na mahitaji kamilifu yanayotosheleza kidato cha Kwanza hadi cha Nne kabla ya kuanza kujenga miundombinu ya Kidato cha Tano na Sita.

Natoa wito kwa Makatibu Tawala Mikoa wawaelekeze Wakurugenzi wa Halmashauri, Miji na Majiji kuhakikisha azma ya Serikali ya kila Tarafa kuwa na shule ya Kidato cha Tano inatekelezwa ili kupunguza idadi ya wanafunzi wanaokosa nafasi. Kutokana na ongezeko la ufaulu wa masomo ya sayansi tunahimiza shule zitakazoanza Kidato cha Tano ziwe na maabara ili kuongeza idadi ya wanafunzi wa tahasusi za sayansi.

Aidha, shule ambazo hazikupangiwa wanafunzi kutokana na mapungufu mbalimbali, Makatibu Tawala wa Mikoa husika wanahimizwa kuwaelekeza Wakurugenzi kusimamia kwa karibu ukamilishwaji wa shule hizo ili ziweze kupokea wanafunzi wa chaguo la pili (Second selection).

Natumia nafasi hii kuwahimiza wadau wote wa Elimu kuhakikisha kuwa shule zote zinazoanzishwa kwa ajili ya kidato cha Tano ziwe za bweni kwa kuwa wanafunzi wa kutwa ni wachache na ni lazima watoke eneo husika. Kwa mfano, mwaka huu shule ya sekondari Buswelu ya mjini Mwanza imekosa wanafunzi kwa kuwa ni ya kutwa na Mwanza kuna shule 3 za kutwa. Hivyo ilikuwa vigumu kupata wanafunzi wa eneo hilo wa kutosheleza shule hizo.

Wakuu wa Shule wahakikishe kuwa wanafunzi wa kidato cha nne wote wanajaza ‘Selforms’ kwa umakini na kwa usahihi ili kurahisisha zoezi la uchaguzi. Aidha, wazazi kwa kushirikiana na walimu wawaelekeze watoto wao kuwa na dira, kuwasaidia kusoma kwa malengo na kufanya machaguo ya tahasusi kulingana na dira walizonazo.

10.0 WANAFUNZI KURIPOTI KATIKA SHULE WALIZOPANGWA

Muhula wa kwanza kwa wanafunzi wa Kidato cha Tano mwaka huu 2014,utaanza mwezi Julai tarehe 10. Wanafunzi wamepangwa katika shule zenye miundombinu na walimu kwa masomo husika. Aidha, iwapo baadae mapungufu yatajitokeza, wakuu wa shule wameelekezwa kutoa taarifa kwa uongozi wa Halmashauri husika kuhusu upungufu huo.

Uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano umefanyika kwa kutumia mfumo wa kompyuta kwa kuzingatia machaguo ya wanafunzi pamoja na ufaulu hivyo hakutakuwa na mabadiliko yoyote.
Kwa nafasi hii, naagiza wanafunzi wote kuripoti katika shule walizopangwa tarehe 10 Julai, 2014. Wanafunzi ambao watashindwa kuripoti shuleni hadi tarehe30 Julai, 2014 nafasi zao zitajazwa na wanafunzi ambao wamekosa nafasi.

Mwisho ninachukua nafasi hii kuwapongeza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi mwaka 2014, walimu, wazazi, Bodi za Shule, viongozi, jamii na wadau wote wa elimu kwa jitihada za kuwaandaa wanafunzi, na kufanikiwa kuingia Kidato cha Tano. Ushirikiano wa wadau wote unatakiwa ili kuboresha elimu hapa nchini.

Wataalam wa elimu kuanzia ngazi ya shule wawe na utaratibu endelevu wa kuelimisha wadau katika utekelezaji wa malengo yanayopimika. Katika utaratibu wa ”Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now)”; kila mmoja anatakiwa kuacha utendaji wa mazoea na afanye kazi kwa malengo na viwango, kuwa na mipango inayotekelezeka ya muda mfupi na muda mrefu na kuwa na vipindi vya tathmini kwa kila lengo kabla, kati na mwisho wa utekelezaji. Ni matumaini yangu kuwa wakuu wa shule na viongozi wote wa elimu wakizingatia taratibu hizi, elimu inayotolewa hapa nchini itaendelea kuwa bora zaidi.

Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2014 inapatikana katika tovuti zifuatazo: -

Ahsanteni kwa kunisikiliza.
Mhe. Kassim M. Majaliwa (MB)
OFISI YA WAZIRI MKUU - TAMISEMI






































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.