.wamepokea shilingi 80 bilioni katika mpango wa makazi kwa watumishi wa umma

Na Damas Makangale, Makangale Satellite 

Kwa watumishi wa umma uanzishwaji wa Watumishi Housing Company (WHC) ambao ni mpango wa makazi kwa watumishi wa umma ni mkombozi wa kweli kwa ustawi wa maisha ya mfanyakazi wa serikali, asante kwa serikali ya awamu ya nne kwa kuanzisha taasisi hii muhimu kwa ujenzi wa taifa.
 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Watumishi Housing Company (WHC), Dakta Fred Msemwa akiwa amepozi ofisini kwake baada ya mahojiano.
WHC ni taasisi inayojihusisha na uendelezaji miliki na usimamizi wa uwekezaji katika miliki. Kampuni hii ya umma imepewa jukumu la kuwa mtekelezaji mkuu wa mpango wa taifa wa makazi kwa watumishi wa umma na ina jukumu la kujenga nyumba 50,000 nchi nzima.
Akizungumza na Makangale Satellite mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji mkuu wa WHC, Dkt Fred Msemwa amesema kuwa nyumba hizo zitauzwa kwa mkopo nafuu wa muda mrefu kwa watumishi wa umma.

“Baada ya Benki Kuu kulegeza masharti ya mikopo ya nyumba kwa hiyo sasa mtumishi wa umma haihitaji fedha ya kutanguliza (deposit) ambayo ni tofauti na masharti yaliyopo sasa katika uuzaji wa nyumba kwa mikopo ambayo yanamtaka mnunuzi atoe asilimia 10 mpaka 20 kama fedha ya utangulizi,” amesema Dkt Msemwa 

Amesema kwamba WHC ni taasisi ya umma yenye jukumu la uendeleza makazi yaliyo bora kwa watumishi wa umma nchini na ilianzishwa mwaka 2013 na jukumu kubwa ni kuboresha na kujenga makazi ya watumishi wa umma nchi nzima.

Dkt Msemwa alisisitiza kwamba serikali iliamua kuja na utaratibu huo wa makazi kwa watumishi wake baada ya kuona kwamba kwenye nguvu ya soko la makazi watumishi wachache wanaweza kumudu nyumba zinazouzwa na taasisi za fedha kwa sababu ya riba kuwa juu.

Amesema kwamba mkopo katika nyumba hizi ni kwa miaka hadi 25 na riba ya nyumba hizi ni asilimia 10 hadi 13 ukilinganisha na hali ilivyo kwenye soko la sasa la nyumba nchini Tanzania.

Dkt Msemwa amesema kwamba ujenzi rasmi wa nyumba hizi za watumishi wa umma zitaanza kujengwa mwezi oktoba mwaka huu sehemu mbalimbali za nchi kama vile Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Arusha, Shinyanga, Mwanza, Tabora, Dodoma, Morogoro, Mbeya, Lindi na Mtwara.

Amesema kwamba inakadiriwa kwamba kuna wafanyakazi 650,000 wanaofanya kazi kwenye mashirika na sekta ya umma ambapo wafanyakazi 10,000 sawa sawa na asilimia 2 tu tu waliopata mikopo ya nyumba.

Aliongeza pia WHC wameweza kufika hapo walipo baada ya kupata Baraka ya kuwa chini ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo ni Mfuko wa PPF, National Social Security Fund (NSSF), Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa Umma (PSPF), LAPF, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Serikali (GEPF), Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Amesema pia kwamba kampuni hiyo ina jukumu la kusimamia vipande vya uwekezaji katika miliki (Real Estate Investment Trusts –REITs).

“kila mtumishi wa umma atanunua nyumba kwa kupitia mkopo kwa kuangalia kiwango chake cha mshahara kama mtumishi wa umma,” alisisitiza
Dkt Msemwa alifafanua kwamba tofauti kati ya WHC ni mabenki na kampuni zingine ni kwamba wengine wanafanya biashara kwa kuangalia faida ila taasisi wana malengo ya kuhakikisha mtumishi wa serikali anapata makazi bora ya kuishi kabla na baada ya kustaafu.

Amesema kwamba kuanzia katika mkoa wa Dar es Salaam nyumba zitajengwa Mabwepande, Magomeni na Kigamboni baada ya kukamilisha taratibu zote kwa kushirikiana na serikali za mitaa na wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi ili kuhakikisha maeneo yote yanakuwa na hati miliki (title deeds).

Dira ya WHC ni “Makazi Bora kwa Watumishi wa Umma” na Dhima kuwezesha watumishi wa umma kumiliki nyumba kwa njia ya mikopo nafuu na kufaidi matunda ya uwekezaji katika miliki kwa kutumia wafanyakazi wenye weledi katika usimamizi wa uwekezaji na uendelezaji miliki.

Mwisho.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.