KATIKA maisha yetu bila shaka tuna watu wengi au wachache ambao toka
moyoni mwetu tunawachukia na pengine tamaa yetu ni kuona wanapatwa na
mabaya kila siku. Miongoni mwao ni marafaki, wafanyakazi na ndugu zetu.

Pamoja na kuwepo kwa chuki ya asili ambayo nayo hufanya kazi kwenye maisha
ya mwanadamu, lakini wengi wetu tuna chuki zinazotokana na orodha ya
mabaya tuliyowahesabia wenzetu.

Mfano Mume anaweza kuwa na orodha ndefu ya matendo machafu ya mkewe tangu
walipooana miaka saba iliyopita, ambapo kila siku anapomtazama tu huwa
kama anatazama CD ya matukio yaliyopita na kuifanya chuki yake kukuwa kila
siku.

Kwa bahati mbaya, wanadamu wengi wako hai kwenye mabaya, uwezo wao wa
kukumbuka makosa ni mkubwa zaidi kuliko wema wanaofanyiwa. Tabia hii
inatokana na ukweli kwamba, akili zina tabia ya kukosoa muonekano na
taarifa ya vitu, lengo ni kuweka ulinganifu wa jinsi mtu anavyojitambua.

Kwa kutambua hilo, kinachotujengea chuki juu ya wenzetu ni ‘USISI’ ambao
kila mtu anao. Wako wenye usisi wa udini, ukabila, rangi, jinsia, uwezo,
elimu na tabia. Hali hii ndiyo inayowafanya wawaone wenzao kama wakosaji.

Unamchukia mumeo kwa sababu unataka awe kama unavyopenda, hupendani na
mfanyakazi mwenzako, jirani yako, mke mwenzako kwa vile unajenga msukumo
wa usisi kwenye mtazamo wako juu yake.

Ifahamike kwamba msingi huu wa maisha ni hatari kwa vile umekuwa mzigo
mzito kwenye maisha ya wanadamu wengi. Watu wengi wamepata matatizo
makubwa kwenye maisha yao kwa sababu walishindwa kujigundua kuwa wana
usisi na hivyo kulazimisha ulimwengu ufanye watakavyo, jambo ambalo ni
gumu.

Ni ukweli ulio wazi kwamba, hatuwezi kuishi kwenye mtazamo wa kutaka
mapenzi yetu yatimizwe na kuwa na msukomo wa lazima wa kuifanya jamii
inayotuzunguka itumikie mtazamo wetu. Kamwe hatuwezi kuwafanya wenzetu,
watembee, waongee, wawe na tabia kama zetu.

Wajibu wetu mkuu kwenye maisha ni kujitambua na kuacha wengine nao
watumikie kujitambua kwao kama binadamu. Tusiingie kwenye uhasama wa bure
kushindania mtazamo. Tukumbuke mpaka tunaondoka duniani hali ya kila mmoja
kujitambua mwenyewe haitafutika.

Mama Teresa aliacha neno la msingi kwenye maisha yetu lisemalo: “If you
judge people, you have no time to love them.” Kama utakuwa mwenye kuhukumu
wengine hutakuwa na muda wa kuwapenda.

Mama Teresa, Mama wa upendo
 
 
 Ni vyema tusiwe wepesi wa kuhukumu badala yake tukubali ubinadamu wa
wenzetu katika maisha.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.