KIUNGO CHIPUKIZI Adnan Januzaj amesaini Mkataba mpya na Klabu yake Manchester United wa Miaka mitano.

Januzaj, mwenye Miaka 18, aliifungia Man United Bao zote 2 walipoifunga Sunderland Bao 2-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England waliyocheza mwisho na hiyo ilikuwa ni Mechi yake ya kwanza tu kuanza kwa Mabingwa hao wa England.

Akiongea mara baada ya kusaini Mkataba huo, Januzaj alisema: “Ni furaha kubwa kusaini Manchester United!”

Meneja wa Man United, David Moyes, ameeleza kuwa Januzaj, ambae alijiunga na Klabu hiyo Mwaka 2011 akitokea Anderlecht ya Ubelgiji, ni ‘Kipaji cha ajabu!’
  
Adnan Januzaj-katokea wapi mpka kupewa mkataba mnono wa miaka mitano (5):

.Mzaliwa wa Ubeljiji mnamo Tarehe 5 Februari 1995 kwa wazazi wazaliwa wenye asili ya kutoka Albania na asili ya kosovo mnamo mwaka 1995.

.Alijiunga na Timu ya vijana ya Anderlecht mnamo mwaka 2005 na kudumu nayo kwa takribani miaka sita (6).

Mnamo mwaka  2011,Adnan alijiunga na na timu ya Manchester United.

Akiwa na timu yake mpaya ya vijana wa Manchester United, Januzaj alizidi aling’ara sana kiasi ambacho kocha mstaafu wa wakati huo Mzee Sir Alex Ferguson alitamka wazi ya kuwa "Adnani ni Mchezaji mzuri mno mwenye uwiano mzuri sana kisoka!".

Wakati Ligi hiyo ikiwa ukingoni na huku Manchester wakuwa taayri washajitangazia ubingwa mapema, Mzee Fergie aliamu kumpanga akiwa benchi katiak mchezio wao wa mwisho dhidi ya Westbromwich Albion (WBA) ambayo ilikuwa ndio mechi ya mwisho  ya Sir Ferguson  kama kocha mara baada ya kutangaza kung'atuka.

Januzaj aliuanza msimu huu mpya chini ya kocha David Moyes katika michezo yake ya kirafiki barani Asia kwenye mchezo dhidi mastaa wa  Hong Kong kwenye ya mchezo wa kirafiki na baada ya hapo kwenye mechi ya ufunguzi wa ligi (Charirty Shiedl Cup) dhidi wa mabingwa wa kombe la FA Wigan Athtletic ambapo Mancehster walifanikiwa kushinda mabao 2-0 huku Adnan akitokea benchi..

Msimu huu, amecheza Mechi za Ligi, dhidi ya Crystal Palace hapo Septemba 14 na Capital One Cup akitokea Benchi lakini Mechi na Sunderland hapo Jumamosi ndio ya kwanza kuanza.
-Januzaj yuko huru kuichezea Belgium, Albania, Turkey na hata England


Mkataba wa sasa wa Januzaj ulitakiwa kumalizika mwishoni mwa Msimu huu kitu ambacho kingemfanya Kinda huyo awe huru kuihama Man United kwa fidia ndogo tu Mwezi Januari kwa vile yuko chini ya Miaka 24.
Mara baada ya kusaini Mkataba mpya utakaomweka hadi 2018, Januzaj alieleza: “Ni kama ndoto! Tangu nitue hapa nilijiona nipo kwenye Klabu sahihi kabisa!”

Ingawa aliwekwa Benchi kwenye Mechi ya mwisho kabisa ya Sir Alex Ferguson Msimu uliopita, chini ya Meneja mpya David Moyes, Januzaj ndio amepata nafasi kubwa ya kucheza ambapo alitokea Benchi na kucheza Mechi ya kugombea Ngao ya Jamii dhidi ya Wigan Mwezi Agosti ambayo Man United walishinda 2-0.

Moyes ametamka: “Ni Kipaji cha ajabu! Ametulia na mwenye uwezo wa kutoka wapinzani na hilo ni jambo kubwa kwa Kijana wa Umri wake!”

Hadi sasa Januzaj hajaamua kwenye Timu ya Taifa atachezea Nchi gani kwani yupo huru kuzichezea Belgium, alikozaliwa, pamoja na Albania, Asili ya Wazazi wake, au Turkey, wanakotoka Babu zake.
Pia, Januzaj, kwa mujibu wa Kanuni za FIFA, ataweza kuichezea England ifikapo 2018 ikiwa atabaki Mkazi wa Nchi hiyo hadi atimize Miaka 23.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.