BOSS Automation Ltd, 

kampuni inayoongoza katika vifaa vya teknolojia za mawasiliano kwa kushirikiana na RICOH kampuni ya kimataifa ya teknolojia zimeungana kibiashara katika kusambaza vifaa na bidhaa mbalimbali za sayansi na teknolojia hapa nchini.Katika ushirikiano huo, 

 
Meneja Mkuu wa Kampuni ya kampuni ya vifaa vya teknolojia za mawasiliano  ya BOSS Automation Ltd Tanzania, Andrew Thompson akikata utepe kuzindua moja ya mashine ya kuchapia na kudurusu aina ya  RICOH wakati kampuni hiyo ikitangaza kuungana kibiashara na kampuni ya kimataifa ya vifaa vya teknolojia ya mawasiliano ya RICOH jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa BOSS, Khalid Yahia na kulia ni Mwakilishi wa RICOH, Tobia Johansson. 
kampuni hizo mbili kubwa katika biashara ya tekonolojia duniani wataweza kusambaza vifaa na bidhaa mbalimbali za uchapaji wa kisasa kwa kutumia teknolojia ili kuleta ufanisi katika ofisi za binafsi, umma na mashirika mbalimbali Afrika Masharikina Kati.


Akizungumza na waandishi wa Habari leo asubuhi jijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa Kampuniya Boss, Andrew Thompson amesema ushirikiano huu utawezesha wao kutoa huduma katika ubora wa hali ya juu katika biashara ya kusambaza vifaa vya teknolojia hapa nchini.


Alisema kuwa ushirikiano huu nimuendelezo mzuri kwenye sekta binafsi hasa kwenye sayansi ya teknolojia ambapo mashirika mbalimbali wataweza kufanya shughuli zao katika mazingira bora zaidi na kusukuma mbele gurudumu la maendeleo kupitia teknolojia habari na mawasiliano. 


“katika dunia ya leo ya biashara, kupunguza gharama katika biashara ni muhimu hasa kwa kutumia teknolojia, tunapambana kwa ajili ya ufanisi, huku mashirika yakijipanga katika shughuli zao kila siku ili kukuza mitaji na uchumi wa kampuni husika,’ 


“ sisi kwa pamoja tuna furaha kujiunga na kampuniya RICOH, ambayo inatumiwa na mashirika mengi duniani, na ushirikiano huu utasaidia mashirika ya kitanzania kukua kwa kasi katika Nyanja za sayansi na teknolojia kwakupunguza gharama na kuongezamapato,” alisema.


Kwa upande wake, Meneja mwandamizi wamaendeleo ya Biashara, Tobias Johansson alisema“tumepata faraja kubwa na sisi ni watu wenye bahati kupata yakusaidia maendeleo ya sayansi na teknolojia hapa nchini.


“pia tunasambaza vifaa vingi vya komputa kama vile scanners, projectors, servers, storage equipments, fax mails, paper shredders, laminating machines, and many more,’ alisema.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.