Shirika la habari la BBC limegundua kuwa takriban watu 50 kutoka Uingereza wana uhusiano na kundi la kigaidi la Al-Shabaab na makundi mengine yanayohusika na ugaidi duniani.
Wapiganaji wa kikundi cha Al Shabab

Wengi walio kwenye orodha hiyo walisafiri kwenda nchini Somalia kupigana kwa niaba ya kundi hilo na wengine kujaribu kuifanya safari hiyo ingawa hawakufanikiwa.


Al Shabaab, ambao makao yao makuu ni Somalia walikiri kuhusika na mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jengo la kifahari la Westgate mjini Nairobi.


Mawakili wa familia ya kiingereza ya mmoja wa watu waliosajiliwa kupigania Al shabaab ingawa aliuwawa baadaye, wanachunguza kifo chake.
Abdukadir Mohamed Abdukadir  ambaye anadhaniwa ndiye muunganishaji mkuu wa wapinaji wa kikundi hicho mjini Somalia na wa wale wa  al-Qaeda mjini Yemen

Majina 47 yaliyokusanywa na BBC yalitoka kutoka kwa watu mbali mbali ikiwemo stakabadhi za mahakamani.Takriban watu 32 kati ya walio kwenye orodha hiyo , wanashukiwa kujiunga na al-Shabaab ili kupigana , wakati majasusi wa Marekani M15 walipowanasa wengine wakijaribu kusafiri kwenda Somalia.



Wengine saba walitajwa katika mahakama za Uingereza kwa kujaribu kwenda Somalia ingawa njama yao ilijulikana na kutibuliwa.


Hali ya washukiwa hao haijulikani lakini wanne bila shaka wameuawa.


Ni pamoja na Tufail Ahmed kutoka Mashariki mwa London. BBC imegundua kuwa polisi waliifahamaisha familia yake kwua alifariki akiwa nchini Somalia mwezi Novemba mwaka jana.

Familia yake imelitaka shirika lisilo la kiserikali la charity Reprieve kuchunguza madai kuwa majeshi ya nchi za Magharibi yalihusika na mauaji hayo,.


Wizara ya ulinzi imekataa kuzungumzia swala hilo.

Wengine walishtakiwa kwa kuchangisha pesa kwa niaba ya al-Shabaab, au kufanya mipango ya kuwasafirisha


Wanne kati ya wanaume hao wamefariki wakiwemo wanaume walioonekana kwenye kanda ya video iliyotolewa na al-Shabaab wiki moja iliyopita.


Mwisho 


Chanzo: BBC Swahili
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.