Na Mwandishi Wetu 
Timu ya CHADEMA ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia Maendeleo (CHADEMA) Zitto Kabwe ametembelea kanda ya Magharibi Mkoa wa Tabora na kumfikisha katika jimbo la Igalula, wilaya ya Uyui.
 

Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia, Mhe Kabwe amekutana na wananchi katika vijiji vya Goweko, Loya, Miswaki, Miyenza na Kigwa.


Kabwe amesema wamezungumza kuhusu changamoto ya usafiri wa reli, wafugaji kunyanyaswa na watendaji wa kata na askari kwa kunyanganywa mifugo yao, zao la tumbaku, maji safi na salama na suala la mchakato wa kuandika katiba mpya.
 

“Kimsingi shughuli za kiuchumi za wananchi ni kubwa na hasa Kilimo na mifugo, hata hivyo ukosefu wa miundombinu unafanya wananchi wasipate thamani ya mazao yao na jasho la kazi zao,” amesema.
 

Amesema alipofika Kijiji cha Loya aliona eneo kubwa lina miti ya mihama ambapo wananchi wanatumia tu mihama wakati wa njaa na mara nyingi matunda haya yanaharibika tu yenyewe.
 


Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe amesema lazima matunda haya yawe na matumizi ya kiviwanda ili kukuza Uchumi na kutoa ajira kwa vijana.


Mwisho.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.