Katika juhudi za kuendeleza sekta ya elimu hapa nchini, Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi, Airtel imetoa vitabu vya kiada kwa shule ya sekondari ya Nyasaka iliyopo jijini Mwanza.

Kampuni hiyo ya simu imetoa vitabu vya sayansi vyenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa shule hiyo iliyopo jijini Mwanza ikiwa ni muendelezo wa mradi wa shule yetu unaoratibiwa na kampuni hiyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vitabu hivyo Meneja Mauzo wa Airtel kanda ya ziwa, Bw. Raphaeli Daudi amesema Airtel inathamini sana umuhimu wa elimu kwenye jamii na ndio maana ilizindua mradi wa shule yetu kwa ajili ya kuzisaidia shule mbalimbali zenye uhitaji wa vitabu.
"Sisi kama kampuni tunaelewa fika jinsi elimu ilivyo na umuhimu mkubwa kwenye jamii, pia tunatambua ni jinsi gani sekta ya elimu inaweza kuleta mapinduzi ya kifikra na ya kiuchumi  kote nchini na ndio maana tunatoa vitabu hivi kwa ajili ya kuendeleza elimu kote nchini" amesema Raphaeli.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Nyasaka, Bw. Yoweri Camilo amesema Airtel ni moja kati ya makampuni yanayothamini elimu kwa ajili ya maendeleo ya jamii na ni kitu ambacho kinapaswa kuigwa kwa makampuni mengine kote nchini.

"Kuchangia sekta ya elimu ni kuiendeleza jamii nzima na Airtel imeweza kutambua umuhimu wa sekta hii na kuiendeleza, Na huo ni mfano wa kuigwa kwa makampuni mengine," alisema Camilo.
Hivi karibuni Airtel ilichangia vitabu mbalimbali za sekondari ikiwemo Kazuramimba ya Kigoma, Kalangalala ya Geita, Kasoma ya Musoma na Buyago ya Bukoba.
Kupitia mradi wa Airtel shule yetu, Airtel mwaka huu imejipanga kutumia zaidi ya milioni 150/- kwaajili ya kusaidia shule za sekondari nchini.

Mwisho
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.