Mkurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Brewers Ltd, Steve Gannon (kushoto) akimpa mkono wa pongezi Linah (katikati) baada ya kukubali kusaini mkataba wa kuwa Balozi wa Jebel.  Kulia ni meneja wa Linah, Tonny Akwesa, akishuhudia makabidhiano hayo

Akizungumza wakati wa makubaliano ya mkataba huo, mkurugenzi wa kampuni hiyo, Steve Gannon, alisema  wameamua kumpatia ubalozi wa kinywaji hicho Linah kufuatia uwezo wake mkubwa katika kuwashawishi wateja wao, na pia hiyo ni njia mojawapo ya kusapoti kipaji chake na itakuwa pia njia ya kushirikiana na wasanii wa Tanzania kwa kila kitu.

“Kampuni yetu imeingia mkataba wa mwaka mmoja na Linah ikiwa njia  ya kutambua sanaa ya muziki Tanzania.   Serengeti Brewers Ltd kupitia kinywaji chetu cha Jebel, tumefurahishwa na uwezo wa Linah hivyo tunaamini kupitia kwake tutaweza kupata manufaa makubwa ya kutangaza kinywaji chetu cha Jebel,” alisema na kuongeza:

“Tunatarajia kuanza naye kazi rasmi kwa kutengeneza video ya wimbo wake mpya ambayo ataifanyia katika nchi ya Kenya na Afrika Kusini.  Video hiyo itakuwa chini yetu, ila mkataba huu utambulike kwamba tunaanza na mwaka mmoja ingawa utakuwa endelevu zaidi.


Linah (kulia) akisaini mkataba  huo na Mkurugenzi wa Serengeti, Steve Gannon, ndani ya ukumbi wa mikutano uliopo katika ofisi kuu za kampuni hiyo Temeke, Chang’ombe, jijini Dar es Salaam.

Linah na Mkurugenzi wa Serengeti Gannon wakionyesha kinywaji cha Jebel.(P.T)

Steve Gannon akiangalia T-shirt yenye nembo ya kinywaji hicho mara baada ya kusainiwa na Lina

Akionyesha T-shirt hiyo baada ya kusainiwa na Linah

Linah akiongea jambo kwa waandishi wa habari baada ya kusaini mkataba



Mkurugenzi Masoko wa Serengeti, Cescar Mloka (wa pili kulia), akifurahia jambo akiwa ameshikilia kinywaji hicho na Linah.  Wengine ni Tonny Akwesa na Steve Gannon


Linah akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Serengeti.


 

Linah akiwa na wafanyakazi wa Serengeti.MSANII kutoka nyumba ya kukuza vipaji Tanzania  (THT) Estelinah Sanga ‘Linah’, leo ameingia mkataba  na Kampuni ya Serengeti Breweries Ltd, kupitia kinywaji chake cha Jebel.
 
”(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)


Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.