Dar es salaam. Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi taifa ,James Mbatia amesema kwamba  ajali  iliyotokea eneo la Mafinga Changalawe mkoani Iringa ilikuwa imepangwa na binadamu na wala sio mipango ya Mungu.
Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kuendelea kwa ajali za barabarani. Picha na Venance Nestory 

Akizungumza jijini leo Mbatia amesema ajali hiyo ilipangwa na watendaji wa serikali  kwa sababu ajali hiyo ilisababishwa na shimo kubwa ambalo limekaa kwa muda mrefu eneo hilo pasipo juhudi zozote za Serikali kulikarabati.
Mbatia amesema hawezi kukaa kimya ni lazima awasilishe suala hili  bungeni ili wahusika wachukuliwe hatua kwa kuacha shimo kubwa barabarani kwa muda mrefu bila kuliziba.
Amesema shimo hilo ambalo ndio hasa lilikuwa chanzo cha ajali hiyo ni la muda mrefu lakini viongozi wa serikali wanaliangalia tu bila kuchukua hatua ya kuliziba.
 ‘’Jamani  watanzania waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo ni wengi na  ni aibu kwa taifa, ukizingatia chanzo cha ajali hiyo ni shimo la muda mrefu ambalo linaangaliwa na viongozi wetu kila siku bila kuliziba’’alisema Mbatia
Amesema ajali hudokeza kwa ujumla matokeo mabaya ambayo labda yangeweza kuepukwa au kukingwa ikiwa matukio yaliyosababisha ajali hiyo yangetambuliwa na kurekebishwa kabla ya tukio.
Amesema madereva wanaoendesha magari ya abiria wanatakiwa kupelekwa shule angalau kwa miezi sita ikiwa ni pamoja na kupimwa afya mara kwa mara.
Aidha ameitaka serikali kutoa tamko kuhusu ajali hiyo na sio kukaa kimya mpaka waanze kupigiwa makelele na wananchi kupitia vyombo vya habari.
Watu  zaidi ya 40  waliokuwa kwenye basi  la kampuni ya Majinjah Express lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam, walifariki papo hapo katika ajali hiyo iliyotokea jana wengine 23 wakijeruhiwa.

Chanzo cha habari na gazeti la kila la mwananchi

























































































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.