Serikali imeamua kuanzisha usajili mpya wa namba za pikipiki (aina zote za pikipiki zenye magurudumu mawili na zaidi) ili kurahisisha usimamizi na utawala wa vyombo vya moto. Utaratibu mpya wa Usajili unaanza rasmi tarehe 1/10/2014. Mmiliki anapewa muda wa miezi sita kubadilisha usajili bila adhabu.

Pikipiki za magurudumu mawili


Usajili huu utahusu vyombo vya moto aina ya pikipiki vyenye magurudumu mawili au zaidi. Pikipiki  kwa ajili ya biashara zinatakiwa kubandikwa vibao vya namba ya rangi nyeupe na kwa ajili shughuli binafsi zitabandikwa vibao vya namba za rangi ya njano.


Usajili huu utafanyika katika ofisi zote za TRA   na mmiliki anatakiwa kwenda TRA na kadi halisi ya pikipiki na Tshs.10, 000/- kwa ajili ya kadi mpya.


Wito unatolewa kwa wamiliki wote wa pikipiki ikiwa ni pamoja na zile za magurudumu matatu au manne maarufu kwa jina la Bajaji, wafike katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa ajili ya kukamilisha usajili wa vyombo wanavyomiliki.
Vyombo vya usafiri vya magurudumu matatu almaarufu kama Bajaj
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.