Tigo Tanzania mkombozi wa wanawake wajasiriamali nchini


Mwaka jana walizindua mpango wa Wezesha Wanawake kwa Maendeleo


Wanawake wengi sasa wameweza kujiendeleza kibiashara na kuhudumia familia zao kwa ubora zaidi.


Na Damas Makangale,  Tanzania  


JUMAMOSI ya kesho, Tanzania itaungana na nchi zingine duniani kuadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake ambapo shughuli mbalimbali zitafanyika katika kutambua mchango wa wanawake kuanzia ngazi ya kaya, taifa na kimataifa.


Siku ya wanawake duniani ni siku ya kimataifa na dunia nzima huadhimisha siku hii ya kipekee kwa kufurahia mafanikio yaliyopatikana kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa upande wakinamama.


Na katika baadhi ya nchikama China, Urusi, Vietnam na Bulgaria siku hii ni mapumziko ya kitaifa na hii yote ni katika juhudi za kutambua mchango wa wakinamama katika kuleta mabadiliko katika jamii.



Ni katika kuadhimisha siku hii muhimu wanawake wote duniani huja pamoja na kutafakari jinsi ya kuendelea kumuelimisha mwanamke na kama usemi maarufu usemao, ukimwelimisha mwanamke ni sawa na kuelimisha jamii nzima.


Hapa nyumbani kwa miaka ya hivi karibuni wanawake wamekuwa wajasirimali wazuri na wenye msaada mkubwa katika familia (kaya) na taifa kwa ujumla.


Siku ya Jumatatu mwezi Julai, mwaka jana, Tigo Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Cherie Blair kwa ajili ya wanawake (CBFW), USAID na FINCA walizindua mpango mkakati wa wanawake wajasiriamali.


Hiyo yote ni kuonyesha ni kwa vipi kampuni hiyo yaTigo Tanzania inavyothamini jamii kwa kuweza kurudisha sehemu ya mapato yake kwa wananchi kupitia kitengo chake cha Huduma kwa Jamii (CR) ili kumwezesha mwananchi wa kawaida na hasa mwanamke mwenye kipato cha chini.


Mpango huo unajulikana kama Wezesha Wanawake kwa Maendeleo, umelenga kuwapa uwezo wanawake zaidi ya 3,200 ambao ni mawakala wa Tigo pesa nchini, kwa kuwapa elimu ya kutunza fedha na kupata masoko katika biashara zao.


Wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Tigo, Diego Gutierrez alisema lengo la mpango huo ni kuwapatia fursa wanawake mawakala wa Tigopesa.


“Kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa, wanawake wanamiliki karibu asilimia 70 ya uchumi wa Afrika, kwa hiyo Tigo inajisikia fahari na heshima kushirikiana na Taasisi ya Cherie Blair, USAID na FINCA katika kutengeneza mazingira ambayo yatawahakikishia wanawake nafasi ya kupata misaada ya kifedha, masoko, mafunzo na mawasiliano ya teknolojia,”

“kwa ushirikiano wetu huu na wenzetu tutaweza kubuni miradi mingi kwa wanawake wa Tanzania pia kuwaongezea fursa za kupata fedha na masoko,” anasema Gutierrez tangu uzinduzi mpaka sasa Tigo imekuwa ikiwapa wajasiriamali hawa mafunzo kuhusu mbinu za kupata mikopo na usimamizi wa biashara ili kuwajengea uwezo wa kusimamia miradi yao kwa maslahi ya kwao na taifa kwa ujumla.



Kwa upande wakinamama wajasirimali, Happy Mabeba, anasema mpango mkakati wa Tigo Tanzania ni faraja kubwa kwa wanawake nchini kwa sababu imemuondoa katika dimbwi la umasikini na utegemezi kwenye familia yake.


Mabeba anasisitiza kwamba kampuni ya Tigo Tanzania na mpango wao wa Wezesha Wanawake kwa Maendeleo ni fursa pekee kwa wanawake nchini ambao tatizo lao kubwa ni mitaji ya kuanzisha biashara mbalimbali.


“Kila mwanamke angependa kuwa na maisha ya kumfanya kuishi bila kutegemea zaidi kwa mwanaume, tumepokea vizuri mpango ule wa Tigo na tunatunaendelea kusogea kutoka tuipokuwa hadi sehemu nyingine nzuri zaidi,”

Na Rose Rwejuna (33) anasema kwamba baada ya Tigo kuanzisha mpango mkakati wa kusaidia wakinamama kupitia bidhaa yake ya Tigopesa maisha ya wakinamama na wasichana wengi yamebadilika kwa kiasi kikubwa.


“baada ya kufungua kibanda changu cha Tigopesa sasa ninaweza kusomesha watoto wangu na kutunza familia bila matatizo yoyote , natoa shukurani za kipekee kwa Tigo,” anasema

Anasema kwamba kwa muda mrefu alikuwa hana kazi ya kufanya wala kipato cha kuweza kujitunza na kutunza familia yake lakini baada ya kampuni ya simu ya Tigo kuanza kusaidia wakinamama amepiga hatua kubwa sana kimaisha.


Zulfa Omari ambaye anamiliki kibanda cha Tigo pesa maeneo ya manzese tip top,  anasema kwamba alipata mkopo kutoka Tigo Tanzania wa fedha taslimu shilingi 300,000  na kuanza rasmi kazi yake ya uwakala mwaka jana mwezi wa Oktoba na inakwenda vizuri.


“kwa kweli napenda nachukua fursa hii adhimu kuwashukuru viongozi wote wa kampuni ya simu ya Tigo kwa msaada wao kwa sababu kwa sasa naweza hata kusomesha watoto wangu wawili mmoja sekondari na mwingine shule ya msingi,” alisema.

Kwa upande wake Dannis Minga yeye ni wakala wa Tigo pesa maeneo ya Ubungo maziwa anasema kwamba alipata mkopo kupitia Tigo wa shilingi 300,000 na kwa sasa ana mtaji wa shilingi milioni moja na lakin tano (1.5m) na ameweza kufungua biashara nyingine ya vipodozi ambayo inamwingizia kipato kwa ajili ya familia.


“yaani sijui nisemeje! Tigo wamekuwa msaada mkubwa sana katika maisha yangu binafsi kwa kunitoa kutoa sehemu moja kwenda nyingine na mshukuru Mungu mwanangu anasoma bila matatizo shule ya msingi sasa,” aliongeza


Katika kuadhimisha siku ya wanawake Jumamosi ya kesho kampuni hiyo ya Tigo Tanzania watagawa zawadi mbalimbali kama mabegi, vocha za bure, T-shirts na peni  katika baadhi ya maduka yake kama vile Mlimani city, Tegeta (Kibo Complex), Quality Mbagala shop, Kigamboni, Mbeya, Tanga na duka jipya Mtwara.


Mwisho.


Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.