Msongamano wa magari jijini Dar es Salaam unaweza kusimuliwa kwa namna nyingi.Ukweli ni kuwa, kila anayeishi jijini hapa ana maelezo yake kuhusu anavyoathirika namsongamano wa magari. Maeneo sugu ya foleni ni yale ya makutano ya barabara kubwa na sehemu nyingine ni zile ambazo huathirika wakati mvua zikinyesha. Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete alieleza kuwa katika kipindi chake cha pili atahakikisha jiji la Dar es Salaam linapata barabara za juu maarufu kama ‘fly-over’.
 

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, barabara hizo zitajengwa katika maeneo ambayo yanakutanisha barabara mbalimbali na maeneo yanayokabiliwa na msongamano mkubwa. Barabara zinazopewa kipaumbele katika ujenzi wa flyovers ni zile za Mwalimu Nyerere na Morogoro. Lakini hizi bado ni kauli tu ambazo hazijaanza utekelezaji hali inayofanya kuendelea kumomonyoka kwa uchumi wa taifa na wa mtu mmoja mmoja. Ni jambo la wazi kuwa idadi ya magari inaongezeka kwa kasi jijini hapa, hali hii inaonesha kwamba watu kumiliki magari sio tena kitu cha anasa bali inatokana na uduni wa usafiri wa umma.

ATHARI ZITOKANAZO NA MSONGAMANO WA MAGARI

Wachangiaji wa mjadala huu wamebainisha athari zitokanazo na tatizo la msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam. Zipo athari nyingi za kiuchumi, kijamii na kimazingira. Imebainishwa kwamba misongamano ya magari inachangia kwa kiasi kikubwa kuporomosha uchumi wa watu binafsi wa taifa na hata kuendeleza umaskini (Dk. Khamis).



Wananchi wanalazimika kutumia kiasi kikubwa cha mafuta (pesa) kutembea mwendo mfupi. “Angalia muda unaopotea barabarani na petroli/dizeli na mafuta mengine ya kulainisha mitambo inayopotea bure hasa ukizingatia kwamba vyote hivi tunaagiza nje ya nchi” ni hifadhi ya fedha za kigeni kiasi gani benki kuu inatumia kununulia bidhaa hizi,” alihoji Festo Maro. Vile vile athari zingine zilizoainishwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira kutokana na hewa mkaa inayotolewa na magari yanayotumia muda mrefu njiani yakiwa yananguruma bila
kutembea. Vile vile watumiaji wa magari hayo hufika katika sehemu zao za kazi na hata majumbani mwao wakiwa wamechoka na hivyo kutokufanya shughuli zao ipasavyo.

Moja ya Barabara za juu almaarufu kama 'Fly Overs"
Ujenzi wa Dar es Salaam mpya

Wachangiaji wengi katika mada hii wanakubaliana na hoja ya ujenzi wa mji mwingine nje ya Dar es Salaam na kuacha mji wa zamani kama ulivyo ili kuhifadhi historia yake kwa vizazi vijavyo. Dk Omari Khamis anasema;”Mji huu mpya ujengwe kwa makini sana ili tuepuke msongamano si wa magari tu bali hata wa nyumba. Ofisi za serikali zisambazwe na kila eneo liwe na huduma zote za kijamii zinazohitajika katika maisha ya kila siku kwa mfano maduka, hospitali, vituo vya polisi, shule na mahoteli n.k”


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi Bw. Mrtin Ntemo




Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi Bw. Mrtin Ntemo akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu maendeleo yaliyofikwa katika ujenzi wa barabara hapa nchini tangu Serikali ya  awamu ya nne ilipoingia madarakani . Kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Frank Mvungi.


Magari ya mradi wa mwendo kasi













Foleni katikati ya jiji, makutano ya Askari monument mauungio ya Barabara maarufu ya Samora jijini Dar Es Salaam.



















































































































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.