BAADA ya kuchapwa Bao 3-1 wakiwa katika uwanja wao waa Emirates na Bayern Munich kwenye Mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE (UCL), Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, anaelekea kukubali kuwa huu utakuwa Msimu wake wa 8 mfululizo wa ukame wa Makombe pale aliposema itakuwa vita rahisi kuwania nafasi ya 4 kwenye English Premier League (EPL), badala ya kutegemea kubaki UCL kwa kuifunga Bayern huko kwao Allianz Arena katika marudiano.

Mara baada ya Mechi hiyo ya Arsenal na Bayern Munich kumalizika, Wenger, alionyesha waziwazi kuumizwa na kipigo na hakupeana mkono na Meneja wa Bayern, Jupp Heynckes, na Wasaidizi wake na kutimkia moja kwa moja Chumba cha Kubadilishia Jezi ambako inadaiwa alikaa peke yake kwa Dakika 25.
Kwenye EPL, Arsenal wapo nafasi ya 5 wakiwa Pointi 4 nyuma ya Timu ya 4 Tottenham na hilo lilimfanya Wenger aibuke toka Chumba cha Kubadilishia Jezi akiamini ni rahisi kuikamata nafasi hiyo ya 4 na kufuzu kucheza UCL Msimu ujao kuliko kupindua kipigo cha 3-1 huko Allianz Arena watakaporudiana na Bayern Mwezi Machi.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.