WIKI iliyopita chama cha Utabibu wa Dawa za Asili Tanzania (ATME) kilifanya mkutano wa kipekee na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kwa lengo la kuangalia namna bora ya kulinda na kuiteteta huduma ya Afya kwa kuelimishana na wahariri pamoja na waandishi wa habari.
 
Mlezi wa Chama Cha Utabibu wa Dawa Asilia Tanzania (ATME), Kingunge Ngombale (kushoto), akifungua mafunzo kwa wahariri na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu tiba asilia, May 15,2014 katika ukumbi wa mikutano NIMR jijini Dar es Salaam,ambapo amewataka Watanzania kuondokana na imani potofu dhidi ya tiba asili na badala yake watumie ili kupona maradhi mbalimbali yanayowakabili (kulia),Mwenyekiti wa Chama cha Utabibu wa Dawa Asili Tanzania (ATME), Bw.Simba Abdulrahmani.
Mgeni rasmi kwenye semina hiyo ya siku moja alikuwa ni Mlezi wa ATME, kingunge Ngombale Mwiru ambaye alichukua nafasi hiyo kusema utafiti ndiyo utakaowezesha kupiga hatua nzuri ya kupata tiba ya maradhi mbalimbali kwa kutumia tiba asilia.
 
Lucey Samwel, kutoka kitengo cha Tiba asilia Wizara ya Afya akiwakilisha mada ya sera ya Afya, Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala, pamoja na taarifa mbalimbali zinazohusu Tiba Asilia na udhaifu katika usimamizi wa sheria ya TATM ya mwaka 2002.
Mzee Kingunge alitumia muktadha huo kusema kuwa kuna dawa nyingi za tiba asilia ambazo zina matokeo mazuri nay a haraka pengine kuliko zile za kisasa, lakini hakuna utafiti wa kutosha nah ii ni kutokana na uhaba wa fedha za kufanyia utafiti.

“tatizo kubwa linalowakabili watafiti wazalendo na hata hawa vijana wa sasa kwenye vyuo vikuu vya tiba na uhaba wa fedha za kufanyia utafiti lakini tukijikita kwenye utafiti maradhi mengi tunaweza kuyaondoa,” amesema Kingunge Ngombale Mwiru
“Kushindikana kwa utafiti kwa sababu ya ukosefu wa fedha kunafanya kukosekana maendeleo na badala yake tutakuwa tunarudia waliyogundua wazee wetu. Tukitaka kwenda mbele lazima kusimamia waliyoyagundua wao na kuendelea mbele,”aliongeza.
 
Mkurugenzi kutoka Paseko T.H.P, Othman Shem.akielezea kuhusiana na Tiba Asili Tanzania na changamoto zake.
Kingunge alisisitiza kwamba ili utafiti ufanyike, ni lazima wawepo watu ambao wana taaluma hiyo na pia wapende fani hiyo na hali hicho ndicho kilichozifanya India, China na Vietnam kupiga hatua katika tiba za asilia na kupunguza kasi ya magonjwa mengi kwenye nchi zao.

“Mathalan, pumu katika hospitali inasemwa kuwa hakuna tiba yake zaidi ya ile ya kutuliza, lakini mtaani unasikia kuna mtu anatibu pumu na pia kuna watu wengi katika maeneo tofauti ambao wanatibu magonjwa mbalimbali, lakini mwendelezo hakuna kwa kuwa hakuna mafungu ya utafiti.”

Amesema vijana wengi wasomi nchini wanafanya utafiti, lakini ni kwa maelekezo ya taasisi za nje kwa kuwa zina fedha za kuwataka wafanye utafiti wa hiki au kile kwa maslahi ya taasisi hizo za nje.

Kwa upande wake, Mwanasheria Onesmo Munuo akiwasilisha mada juu ya mapungufu ya usimamizi wa sheria na 23 ya 2002 pamoja na kanuni zake na madhara yanayotokana na udhaifu wa usimamizi huo amesema shirika la afya duniani linakadiria kuwa Tiba Asili inatoa huduma kwa asilimia 80 ya wanaohitaji huduma za afya katika nchi zinazoendelea.

“Hapa kwetu Tanzania inakisiwa kuwa asilimia 60 ya watanzania wanatumia tiba asili katika kutibu magonjwa yao na kwamba kila kijiji kina watoa huduma wa tiba asili,”
“hili linaonekana pia katika Sera ya Afya na Ustawi wa Jamii inaposema kuwa takribani asilimia 60 ya wananchi huanza kutumia tiba asilia wanapopatwa na maradhi kabla ya kwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya,” alisisitiza Munuo
 Amesema kwmba, kwa tafiti zilizofanyika hivi karibuni, tiba asili na dawa asili ndicho chanzo pekee kinachoonyesha uwezo wa kutoa aina mpya ya dawa kwa matumizi ya sasa kwa matumizi yajayo.

Munuo aliongeza kwa mujibu wa kitabu kilichoandaliwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala “TIBA ASILI KWA JAMII mwezi Aprili mwaka 2009 kinasema kibiashara, soko la dawa za asili duniani kwa mwaka 2004 lilikuwa dola za kimarekani bilioni 60.

Amesema kwa sasa inakadiriwa kufikia mwaka 2050 soko la Tiba Asili na Tiba Mbadala litakuwa dola za kimarekani trilioni 5 na hapo ndio utaona mchango wa tiba asili kwenye uchumi wa dunia.

Aliongeza kuwa sifa za kusajiliwa ni lazima mtu awe na umri wa miaka 18 au zaidi na anatoka katika familia ya mganga au mkunga ambako atakuwa amepewa mafunzo ya uganga au ukunga wa tiba asili na siyo vinginevyo.
Kwa mujibu wa Dkt Othman Shem kutoka Paseko Natural Health Clinic anasema kwamba Tiba Asili dnio tiba mama na kongwe kulio tiba zote duniani iliyoanza kupambana na maradhi yanayo msumbua binadamu.

“Tiba asili huchangia matibabu ya binadamu duniani zaidi ya asilimia 60 hadi 80 hizi ni takwimu za Shirika la Afya Duniani,”
“kwa kusisitiza ni kwamba Tiba asili ndio chanzo cha tafiti nyingi za madawa zinazofanywa na tiba zingine kama tiba mbadala na za kisasa,” amesema
Awali, Mwenyekiti wa ATME, Simba Abdulrahman Simba amesema kuna dawa nyingi za tiba za asili ambazo zina matokeo mazuri kuliko inavyofikiriwa na akaitaka Serikali kuruhusu dawa za jadi kutolewa hospitalini kama ilivyo nchi nyingine duniani.
 
Mwanasheria kutoka AUDA, Onesimo Munuo (kushoto), akielezea mapungufu ya utekelezaji ya Tiba asili na mbadala

Wahariri na waandishi kutoka vyombo mbalimbali waliohudhuria mafunzo hayo




Mlezi wa Chama Cha Utabibu wa Dawa Asilia Tanzania (ATME), Kingunge Ngombale. Akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo


Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.