KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo Tanzania, leo imezindua tamthilia ya ‘Kinga ya Moyo Wangu’ itayokuwa inarushwa hewani kila siku kwa wiki nane na kituo cha utangazaji cha Clouds FM ambacho kitatoa elimu na kuhamasisha watumiaji wa simu za mkononi wa mtandao wa tigo kujiunga na bidhaa ya pona na Tigo bima.
 
Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Diego Gutierrez (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa tamthilia ya redio iitwayo ‘Kinga ya Moyo Wangu’ itakayoelimisha watanzania kuhusu umuhimu wa bima jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Mkazi wa Kampuni ya BIMA inayotoa huduma za bima kupitia simu za mkononi, Christian Karlander.  Tamthilia hiyo itasikika katika vipindi vya Jahazi na Leo Tena vya Clouds FM.
Akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez amesema tamthilia hiyo maridhawa yenye matukio ya kusisimua itawavutia wasikilizaji pamoja na kuwaelimisha watanzania kuhusu manufaa ya bima.
 
“Kampuni ya simu za mkononi kama Tigo ina wajibu katika kuwapatia wateja wake huduma na bidhaa zenye gharama nafuu. Sambamba na jinsi teknolojia ilivyoweza kuleta mageuzi katika namna ambavyo tunaweza kutuma na kupokea fedha barani Afrika,”
 
“hivi sasa tupo tayari kufanya hivyo kupitia bima ya simu. Tigo inayofuragha kuwa mstari wa mbele katika hatua hii kubwa kwa ajili ya Tanzania, ukuaji wa uchumi wake na maendeleo ya taifa nzima,” amesema Gutierrez
 
Meneja Mkazi wa Kampuni  inayotoa huduma za bima kupitia simu za mkononi  ya bima Tanzania, Christian Karlander (kulia) akionyesha kipeperushi wakati wa uzinduzi wa tamthilia ya redio iitwayo ‘Kinga ya Moyo Wangu’ itakayoelimisha watanzania kuhusu umuhimu wa bima jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Diego Gutierrez.
Amesema kwamba programu hiyo ya redio imefadhiliwa na benki ya maendeleo ya Umoja wa Ulaya kwa ajili ya kuelimisha umma umuhimu na faida ya kuwa na bima wakati wote.
 
Kwa upande wake , Meneja Mkazi wa Bima Tanzania, Christian Karlander amesema kuwa tamthilia hiyo itarushwa mara mbili kwa siku kwa muda wa wiki nane kupitia vipindi vya Jahazi na Leo Tena.
 
“Mradi huu umezinduliwa na Bima, Kampuni inayoongoza kwa kutoa bima kupitia teknolojia ya simu za mkononi nchini Tanzania, ambayo inatoa huduma ya bima ya maisha nay a kulazwa hospitalini jijini Dar es Salaam kupitia mtandao wa simu wa Tigo,” amesema
 
Karlander aliongeza kuwa takribani milioni 4.6 ambayo ni asilimia 19 ya watu wazima nchini wamewekewa bima, lakini ni kupitia bima za waajiri wao au chini ya mikopo hata hivyo, kiwango cha watanzania waliojiandikisha bima kwa hiari ni ndogo sana.
 
“Jijini Dar es Salaam, Bima imesajili zaidi ya wateja 500,000 baada ya miaka miwili tu ya kuanza kufanya kazi nchini, na asilimia 79 ya wateja hao ni watu wenye vipato chini ya dola 2.50 (shilingi 4,215) kwa siku,” aliongeza Karlander
 
Meneja Usambazaji wa Kampuni  inayotoa huduma za bima kupitia simu za mkononi  ya bima Tanzania, Donald Galinoma (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamthilia ya redio iitwayo ‘Kinga ya Moyo Wangu’ itakayoelimisha watanzania kuhusu umuhimu wa bima jijini Dar es Salaam jana. katikati ni Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Diego Gutierrez.
Alisisitiza kuwa bidhaa hiyo ya bima kuanzia gharama ya shilingi 750 na kiwango cha juu ni shilingi za kitanzania 4,000 kwa mwezi na Bima inalipa mpaka shilingi 600,000 pindi mteja anapolazwa hospitalini au kufariki dunia.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.