KAMPUNI ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ya Shanta Mining Ltd imetoa leseni tatu na mtaji wa shilingi milioni 40 kwa kikundi cha wachimbaji wadogo cha Aminika cha kijiji cha Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida.


Kikundi hicho Aminika Gold Mine Co- Operative Society Ltd Mang’onyi, kimekabidhiwa leseni hizo hivi karibuni na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stepheni Maselle kwenye kijiji cha Sambaru.


 Akikabidhi leseni hizo Naibu Waziri Maselle amewataka wanakikundi kujipanga vizuri katika kuanza kufanya kazi ya uchimbaji dhahabu ili kujikwamua kimaendeleo.


Aidha amesema ni matarajio yake kuona kuwa kikundi hicho kinakuwa na maendeleo na kuwa mfano wa kuigwa hapa nchini kwani tayari nguvu kazi wamepewa mtaji na Shanta.


 “Ndugu zangu sijui Mungu awape nini mmepewa leseni, mmepewa mtaji na vifaa vya kuanzia kazi na hawa wenzetu wa Tan Discovery mnaoneshwa eneo ambalo tayari limefanyiwa utafiti, sasa kazi kwenu.” Amesema Maselle huku akishangiliwa na wananchi.


Aidha aliwataka wanakikundi hao kutumia kama SACCOS katika kukopa sehemu mbalimbali za kifedha kwa manufaa yetu na kizazi cha baadae.


Hata hivyo Naibu Waziri, Maselle amesema ni dhamira ya serikali kuendeleza wachimbaji wadogo hapa nchini kwa kuwapatia mafunzo na namna bora ya uchimbaji madini.


Katika risala ya wanakikundi cha Aminika iliyosomwa na Katibu wake, Hamis Kingi amesema kikundi hicho ni  muungano wa vikundi  vitano kutoka vijiji   vitatu vitakavyoathirika na Mgodi wa Kampuni ya Shanta Mining vyenye jumla ya wanachama 218.


Kingi alivitaja vikundi hivyo kuwa ni Elimika  Sambaru,Amani Sambaru, Amka Sambaru, Aminifu Mang’onyi na Muungano Mlumbi ambavyo kwa pamoja vimeungana   na kuwa kikundi kimoja kinachojulikana kwa jina la Aminika


Aidha alitanabaisha kwamba vikundi  baada ya maelekezo  hayo   ya Serikali wachimbaji waliendelea kujiunga pamoja na kuunda  kikundi kilichofuata utaratibu wa kisheria wa kusajiliwa na kupata usajili namba, SIR624  Kikundi  cha Aminika Gold Mine  Co – Operative  Society Ltd – Mang’onyi  hatimaye  wamekabidhiwa   rasmi na Serikali.


 “Mh,Naibu Waziri wa Nishati na Madini kwa kuwa kikundi  kiko Kisheria  tunaomba  Serikali  kupitia  Wizara yako ya Nishati na Madini Makubaliano yetu kati ya Kampuni na  Kikundi cha Aminika yaweze kutekelezeka  kwa muda  mwafaka, kwani  wanakikundi  wanahitaji kufanya  kazi  ili kujikwamua kiuchumi.”Alifafanua Kingi.



“Pia tunakushukuru wewe  binafsi kwa juhudi zako  kubwa kuwatetea  wachimbaji wadogo kwa kupitia Wizara ya Nishati na Madini.” Amesema.

Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.