WATANZANIA taratibu wameanza kuona kama ni mchezo wa kuigiza au mazoea pale kila baada ya muda fulani tukio la kulipuka kwa bomu katika kanisa au sehemu ya mkusanyiko au kwenye mkutano wa kisiasa kama ni jambo la kawaida.
 
Tukio la bomu katika kanisa Arusha

Imefikia mahali kwamba milipuko ya mabomu inaanza kuonekana kama ni sehemu ya utamaduni wetu kwa kukubali kwa kirahisi watu wenye dhamira ovu na katili ya kutaka kuangamiza binadamu wenzao pasipo sababu ya msingi na hata kama mtu ana sababu ya msingi kuelezea hisia zake juu ya jambo fulani lakini si kwa njia ya kutoa roho ya mtu mwingine.


Imekuwa kama mazoea kwa baadhi ya makundi ya watu kutumia imani (dini) kuelezea hisia zao kali kwa kushambulia sehemu ya imani nyingine hii kwa kweli kwa jamii iliyostarabika haikubaliki hata kidgo tena kwa watanzania waliozoea kuishi pamoja bila kujali tofauti zao za rangi, dini, kipato, itikadi au tofauti zozote wamekuwa wamoja tangu uhuru.


Na ndugu msomaji watanzania hawa wamekuwa wamoja tangu enzi na enzi na waasisi wa taifa hili yaani Baba wa taifa, Mwl Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume waliweza kwa nguvu zao zote kuwaunganisha watanzania na kuwa kitu kimoja bila mifarakano yoyote ndani ya jamii.


Sisi Moblog tunapenda kuchukua nafasi kuwaambia watu, mtu au kikundi cha watu au magaidi kwamba watashidwa kwa nguvu ya dola na mwenyezi mungu kwa mipango yao ya kiovu kutaka kutoa roho za watu wasio kuwa na hatia.


Lakini kama kuna kikundi cha watu kinajificha kwenye kichaga cha imani kutaka kuelezea hisia zao kwa kuwaua watu wengine yaani watu wenye misingi au imani kali za kidini(Religious Fanaticism) kwa kweli ni upofu wa kutokuona mbali kabisa lakini vyombo vya dola lazima viwajibike haraka na kuwashughulikia kwa ukamilifu vikundi au kikundi kama hivi hapa nchini.


Tunasema mapema kwa kuvikumbusha vyombo vya dola kwa sababu  imani kali za kidini zikiachwa kama ule msemo usemao ‘mchelea mwana kuliwa matangani’ kama kule Nigeria ambapo kilundi cha kigaidi cha Boko Haram kinavyowatesa wananigeria na viongozi wao. 


Tumesema hayo tukijua kwamba juzi tu mtu mmoja amejeruhiwa baada ya kulipukiwa na kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kwemye kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Ziwa Victoria, Makongoro Misheni, Mwanza.


Ambapo aliyejeruhiwa ni mhudumu wa nyumba ya wageni ya kanisa hilo, Benadeta Alfred (25) aliyekubwa na mkasa huo juzi saa mbili usiku.


Huo ukiwa ni muendelezo wa matukio kama hayo katika sehemu mbalimbali hapa nchini hususani jijini Arusha chonde chonde Jeshi la Polisi nchini chukueni hatua mapema ya kudhibiti hali hii isifike mahali tukajuta kama nchi na watu wake.


Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.