KAMPUNI ya Saruji ya Tanga (TCCL) kupitia Bodi yake Wakurugenzi imeidhinishga gawio la hisa la shilingi za kitanzania bilioni 7 kwa wanahisa wake baada ya kupata faida ya shilingi bilioni 32,456,234 kwa mwaka 2013.
Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Saruji Tanga (TCCL), David Lee ( wa pili kushoto) akisoma taarifa za fedha za kampuni hiyo wakati wa mkutano wa 20 wa mwaka wa wanahisa wa kampuni hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Cement, Reinhardt SwartMwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Lawrence Masha, na mjumbe mwingine wa bodi hiyo, Dr. Stephan Olivier.

Akizungumza wakati wa Mkutano wa 20 wa Mwaka wa Wanahisa wa kampuni hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Lawrence Masha alisema katika kipindi cha mwaka jana kampuni ya Tanga cement iliweza kutimiza baadhi malengo muhimu na mafanikio katika utekelezaji wa mkakati wake wa kuishi kufuatana na chapa yake na ahadi yake ya kuwa kivutio cha taifa.

“Bodi imependekeza gawio la shilingi 60 kwa kila hisa kwa mwaka 2013,  (2012 ilikuwa shs  55) ikipelekea kiasi cha jumla kwa gawio la shilingi za kitanzania bilioni 3.3 na hii inaleta gawio la jumla kwa mwaka la shs 110 kwa hisa (2012 ilikuwa shs 100) hivyo kufanya jumla ya shs bilioni  7  kwa mwaka mzima,” 

“Tunayo fahari kwa mchango wetu kwenye maendeleo ya Tanzania na muhimu zaidi kwa maisha ya watu wengi ambayo tunaweza kuyagusa na kuyaboresha kutokana na shughuli zetu za biashara,” alisema Masha.
Akizungumza changamoto zinazoikabili sekta ya biashara ya saruji nchini, mwenyekiti huyo aliendelea kuelekeza kilio chao cha muda mrefu sasa dhidi ya saruji inayoingizwa nchini bila kufuata taratibu za sheria za nchi
Masha alilisitiza umuhimu wa serikali kuingilia kati na kuzuia uigizaji wa saruji kwa njia za panya kwa sababu inaua soko kwa watengenezaji wa saruji wa ndani, kuleta bidhaa ambazo zipo chini ya kiwango na pia kuinyhima serikali pato litokanalo na kodi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Cement, Reinhardt Swart alisema kwamba mwaka jana uchumi wa Tanzania ulikua kwa asilimia saba ukachochea zaidi  maendeleo ya kiuchumi ndani ya nchi.
“Mahitaji ya saruji kwa nchi jirani pia yalibaki kuwa juu na kupanua wigo kwa kampuni katika kusambaza bidhaa hizo katika nchi za Rwanda, Burundi, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo,” aliongeza
Aliahidi kwamba kampuni ya Tanga cement itaendelea kusaidia jamii kwenye maeneo ya afya, elimu, maendeleo ya jamii na mazingira na kwa mwaka jana pekee walitumia kiasi cha shilingi milioni 324 kwenye miradi mbalimbali ya jamii.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.