Bingwa mara saba wa mashindano ya baiskeli yajulikanao kama Tour De France, Lance Amstrong amepoteza kila kitu yakiwemo mataji saba  aliyokuwa ameyashinda pamoja na mikataba, kufungiwa kujihusha na mashindano hayo kwa maisha na  makampuni yaliokuwa yanamdhamini mara baada ya kugundulika alikuwa anatumia madawa ya kuongeza nguvu na yaliokatzwa michezoni na idara ya kuzuia utumiaji madawa haramu ya United States Anti-Doping Agency (USADA).

Mwanamichezo huyo anayetokea katika jimbo la Texan nchini Marekani alipatwa na kashfa hiyo mara baada ya idara hiyo kutoa ripoti yake mwishoni mwa mwezi uliopita  na kuonyesha Amstrong amekuwa na tabia ya kutumia madawa hayo na hivyo kufungiwa maisha katika kujihusisha na mashindano hayo tena.

Itakumbukwa Amstrong aliibukia mnamo mwaka 1999 mara baada ya kupona katika ugonjwa wa Kansa  na kujishindia mataji saba mfufulizo. 


Lance Armstrong
alilala tajiri kaamka maskini, Kampuni ya miwani ya  Oakley imekuwa kampuni ya hivi karibuni kusitisha  mkataba na bingwa huyu wa zamani mara baada ya makampuni mengine ya Nike, Trek ya Anheuser-Busch kufanya hivyo wiki iliyopita.


Lance Amstrong enzi zake katika kutesa katika mashindano ya baiskeli


hakuna kama mimi, Lance Amstrong



































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.