Ndugu wanahabari, 
Kufuatia hali tete 
inayowakabili watetezi wa haki nchini Tanzania, mtandao wa Watetezi wa 
Haki za Bidamu Tanzania (THRD) umeamua kuwakutanisha wadau muhimu katika
 utetezi wa haki za binadamu, asasi mbali mbali za kiraia na viongozi wa
 dini ilikujadili namna ya kuzuia wimbi la vitendo vya kikatili na 
ugandamizaji wa haki za binadamu kwa ujumla.
Ni kwa kuzingatia muktadha huu Mtandao wa Watetezi umeandaa kongamano la siku moja litakalojadili
 hali ya haki za binadamu nchini Tanzania, uhuru wa kupata habari na 
tishio la usalama kwa watetezi wa haki za bindamu litakalofanyika katika
 viwanja vya Mtandao wa Jinsia (TGNP) Mabibo Dar 
es Salaam siku ya Jumatano tarehe 12 Septemba, 2012 kuanzia saa 4:00 
mpaka saa 7:00 mchana.
Kongamano hilo linakuja 
wakati familia nyingi wakiwamo akina mama na watoto wakiwa hawajui 
maisha yao ya baadaye yatakuwaje baada ya kufiwa na wapendwa wao 
wakiwamo wazazi ambao bado walikuwa wanahitajika katika malezi ya 
familia zao.
Matukio ya hivi karibuni kabisa yamewahusisha 
mashabiki na wapenzi wa chama kikuu cha upinzani kwa sasa Chama cha 
Demokrasia na Maendeleo kwa upande  mmoja na Jeshi la Polisi kwa upande 
mwingine.
Ipo hatari ya wazazi kuanza kuwazuia watoto wao 
wasihudhurie kabisa mikutano ya chama hicho, lakini kwa upande mwingine 
ipo hatari ya wanachi kupoteza imani na Jeshi la Polisi ambalo kimsingi 
linawajibu mkubwa wa kulinda usalama wa raia na mali zao. Na zaidi ya 
hayo iwapo watu wataanza kuamini kwamba jeshi hilo linatumika kisiasa 
basi ipo hatari ya kuibuka kwa vyombo vingine vitakavyojivisha jukumu la
 kuwalinda Watanzania na mali zao.
Kwa lengo jema la kurudisha 
imani ya wananchi kwa jeshi lao, kwa wanaharakati za binadamu kuendelea 
kufanya kazi bila vitisho na kwa waandishi wa habari kuhakikishiwa 
usalama wao kazini, wadau wote wakiwa ni wanazuoni katika fani za 
habari, sheria, haki za bainadamu na walaji wote wa kazi za habari 
wanaombwa kuhudhuria na kutoa michango ya mawazo yao.
Historia 
inaonyesha kwamba kumekuwapo na mauaji yanayohusiha wanasiasa kama 
ifuatvyo; Arusha katika sakata la kumpinga meya wa mji huo ambapo watu 
watatu waliuawa, Igunga, Singida, Morogoro na tukio la hivi karibuni 
kabisa la mauaji ya kinyama ya mwandishi wa habari wa televisheni ya 
Channel Ten, Daudi Mwangosi.
Matukio mengine ni lile la kutekwa 
kuteswa na kIsha kutelekezwa porini kwa Daktari Stephen Ulimboka 
aliyekuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za wagonjwa na madaktari, 
na pia lipo tukio la kufungiwa kwa gazeti huru la uchunguzi la 
Mwanahalisi.
Wote mnakaribishwa.
Imetolewa na sekretariati ya THRD,
ELIAS MHEGERA- 0754-826272
KAIMU MRATIBU.
WASEMAJI
1.   MISA-TAN
2.   TGNP
3.   MCT
4.   TEF
5.   MOAT
6.   LHRC
7.   UTPC
8.   Jenerali Ulimwengu (bado anatafutwa kwa hilo haja-confirm)
9.   Prof Issa Shivji (bado anatafutwa haja-confirm)
Post a Comment