Na Mwandishi Wetu, Mbeya.
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ameipongeza Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kutokana na bia ya Safari Lager kutwaa Tuzo ya Bia Bora Afrika.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro akizungumza na wananchi wa Mji wa Mbeya wakati upokeaji Tuzo za Bia ya Safari Lager mkoani kwake jana ikiwa ni ziara maalum ya Tuzo hizo kusherehekea pamoja na Watanzania Ushindi wa Bia hiyo ya Kitanzania barani Afrika.Ziara ya Tuzo za Bia ya Safari Lager inayozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL)  ilikuwa Mkoani Mbeya. Kushot ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo (Picha na Mpigapicha wetu).
Kandoro alimwaga sifa hizo wakati akipokea kombe la ushindi huo ambalo lilioneshwa mahususi kwa wakazi wa Mbeya, katika sherehe zilizofanyika kwenye Viwanja vya Kabwe vilivyopo Mwanjelwa mjini hapa jana.
 
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akimkabidhi rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro (kulia) Tuzo za Bia ya Safari Lager ilizoshinda katika mashindano ya Bia Afrika yaliyofanyika nchini Ghana. Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa ziara maalum ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kuonesha Tuzo ilizoshinda Bia yake ya Safari Lager ambapo jana walikuwa Mkoani Mbeya. (Picha na Mpigapicha wetu).
Alisema ni faraja kubwa kwa Watanzania kutokana na bia ya Safari Lager kutwaa tuzo hiyo na kufanikiwa kuzishinda bia zote barani Afrika kwa ubora.
 
Wakazi wa Mji wa Mmbeya wakiwa wamefurika kwa wingi wakishuhudia Burudani na Tuzo mbili zilizotwaliwa na Bia ya Safari Lager inayozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika mashindano ya Bia Afrika yaliyofanyika Nchini Ghana. (Picha na Mpigapicha wetu
“Tunashukuru tumeletewa kuliona kombe mlilolipata kutokana na ubora wa bia yenu, hii ni furaha kwa Watanzania na naamini ushindi huu utachochea watu kupenda bidhaa zao.


“Kufanikiwa kutwaa Tuzo ya Bia Bora Afrika si kitu kidogo, ni faraja kwetu sote na sasa tunaweza kujivunia kile kilicho chetu,” alisema Kandoro.
Sherehe hiyo ya kulionyesha kombe kwa wakazi wa Mbeya kuliambatana na burudani za kila aina, ambazo zilitolewa na vikundi kadhaa vya muziki.


Akizungumzia ushindi huo, Meneja wa bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo alisema ni wa kujivunia zaidi na wao watahakikisha wanaendelea kuzalisha bidhaa bora zaidi.
Safari Lager imefanikiwa kushinda tuzo hiyo, kutokana na shindano lililofanyika Accra, Ghana na kushirikisha bia zote zinazozalishwa barani Afrika.















Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.