Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.

                Makumbusho ya  kabila la Wasukuma eneo la Kisesa  Magu  mkoani Mwanza.
 Kanisa lililojengwa kwa ajili ya kumbukumbu ya makanisa ya kale yaliyojengwa enzi za ukoloni  yapata   miaka  100 ambapo watemi wa kabila la wasukuma walikuwa wakiabudu .
 Ni kama kigoda vile umbo la jengo hili ambako ndiko kulitumika kuhifadhi  ngoma za asili zilizotumiwa na wanasanaa wa kabila la Wasukuma katika koo mbalimbali ngoma hizi zimehifadhiwa yapata miaka 100 sasa .
   Mdau   Madata Ndelule   Charles   mhifadhi    mwandamizi  wa   makumbusho  hayo  akionyesha    mfano wa nyumba   ambayo    watemi    waliishi.
 Bagika na Bagalu ni ngoma za pande mbili ndani ya kabila la Wasukuma ambapo Bagika walikuwa wakicheza ngoma inayoshirikisha nyoka na Bagalu walikuwa wakicheza ngoma inayoshirikisha zana kama majembe ya mkono, zana za kale za kivita.
                                                             Kikundi cha sanaa cha Bujora group
 Zana na nyenzo za enzi za kale zilizotumika katika usagaji nafaka ili kupatikana unga.
       Hatua kwa hatua usagaji nafaka kwa kutumia zana na kale huku nyimbo asili zikitawala .



 Habari na picha kwa msaada wa blogu ya http://netnewstz.blogspot.com
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.