Askari polisi wasio waaminifu wameendelea na tabia ya kuwabambikizia kesi watu hasa wafanya biashara mbalimbali katika maeneo ya kawe.
Askari hao ambao kushirikiana na baadhi ya matapeli na kumfuata mtu na kumuelezea matatizo kama vile kufiwa, kuuguliwa na mgonjwa na kuomba msaada wa kiasi Fulani cha pesa pamoja na dhamana kama simu, komputa, redio, luninga na kadhalika.
Katika utapeli huo wa baadhi ya Polisi na matapeli hao pindi mtu anapoonyesha dalili ya kutokuamini kuja na vitu hivyo kama mdhamana wa kupewa msaada wa kifedha.
Akizugumzia tukio hilo mmoja wa waathrika (jina tunalo) alisema baada ya muda au siku moja kurudi tena akiwa amekamatwa na polisi na kwa madai kwamba vitu alivyoweka kama dhamana vilikuwa ni mali ya wizi
Baada ya songombigo hilo Polisi wanachukua uamuzi wa kuwakamata wote pamoja kwa madai ya kukutwa na vitu vya wizi na kupelekwa kituoni.
Baada ya kufika kituoni utaambiwa kuwa Yule mtu aliyekupa ule mzigo anaendelea kuonyesha sehemu nyingine alikopeleka mali nyingine na wewe utawekwa ndani kwa ajili ya kupelekwa mahakamani ukaunganishwe na wenzako waliouziwa au kupewa mali za wizi.
Baada ya hapo ndipo hudai kiasi kikubwa chja pesa kati ya shilingi laki tano  (500000)- milioni moja (1000000) ili waweze kukuachi huru
Ni watu wengi sana wamekumbana na utapeli huu ambao hufanywa na askari wa jeshi la polisi ambao sio waminifu na kuendelea kulitia doa jeshi la polisi  nchini
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.